Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania(TFF)na Kampuni ya Bia ya Serengeti (SBL) Leo Jumatano Januari 10,2018 wamesaini mkataba wa miaka mitatu wa kuidhamini Ligi Kuu ya Wanawake (WPL) kupitia Bia ya Serengeti Litemkataba wenye thamani ya shilingi milioni 450.
Mshambuliaji Romelu Lukaku aliamua kuondoka Everton baada ya ujumbe wa ''uchawi'' kumwambia ajiunge na Chelsea kulingana na mwenye hisa mkuu wa klabu ya Everton.
Mchezaji huyo wa Ubelgiji mwenye umri wa miaka 24 baadaye alijiunga na Manchester United kwa dau la pauni milioni 75 msimu wa uhamisho uliopita.
Farhad Moshiri aliwaambia wenye hisa katika mkutano na wachezaji kwamba mchezaji huyo alipokea ujumbe ''wa kwenda kuhiji Afrika'' wakati ambapo alitarajiwa kutia saini mkataba mpya katika klabu ya Everton.
''Alikuwa na uchawi na akapokea ujumbe aliotaka kwenda Chelsea'', alisema Moshiri.
Mabingwa wa ligi ya Uingereza Chelsea walikuwa wamewasilisha ombi la kutaka kumsajili Lukaku lakini badala yake akajiunga na Manchester United.
Mwezi Machi ajenti wa Lukaku Mino Raiola alikuwa amedai kwamba mkataba mpya wa kusalia Everton ulikuwa umekamilika asilimia 99.9.
''Tulimpatia kandarasi nzuri zaidi ya Chelsea na ajenti wake aliwasili kuja kutia kandarasi'' , Moshiri aliambia mkutano wa kila mwaka wa Everton.
Bilionea huyo wa Iran, Moshiri ambaye alikwa amewekeza dola milioni 150 katika deni la klabu hiyo, alisema kuwa Everton ilimpatia mshambuliaji huyo fedha nyingi ili kusalia.
''Swala la Lukaku halikuwa la kifedha. Iwapo nitaendelea kuwa miliki mkuu wa klabu hiyo maswala ya kifedha hayatakuwa tatizo''.Moshiri alisema kuwa Lukaku baadaye alimpigia simu mamake kabla ya mchezaji huyo kufichua kwamba alipokea ujumbe uliomwambia ajiunge na Chelsea.
Mshambuliaji wa Chelsea Eden Hazard atashiriki katika mechi dhidi ya Arsenal katika awamu ya kwanza ya nusu fainali ya kombe la Carabao siku ya Jumatano baada ya kupona jereha.
Mchezaji mpya aliyesajiliwa kwa pauni milioni 15 kutoka Everton Ross Barkley hatoshiriki kwa kuwa bado anauguza jereha la nyuma ya goti.
Mkufunzi wa Arsenal Arsene Wenger ataendelea na marufuku ya kutokalia eneo la wakufunzi uwanjani na badala yake kukaa katika viti vya mashabiki huku kikosi chake kikirudi baada ya kufungwa na klabu ya Nottinham Forest katika kombe la FA.
Granit Xhaka anauguza jeraha la kinena huku Shkodran Mustafi ambaye aligongwa akiwa hajulikani iwapo atashiriki.
Mfumo wa kiteknolojia wa video ya kumsaidia refa VAR utatumika katika awamu zote mbili za nusu fainali hiyo.
Arsenal haijashinda kombe hilo kwa kipindi cha miaka 25 huku Chelsea ikiweza kushinda mara ya mwisho 2015.
Meneja wa Chelsea Antonio Conte amesema 'hatausahau' mzozo ambao alikuwa nao na meneja wa Manchester United, Jose Mourinho akiongeza kwamba hiyo ni shida miongoni mwao hao wawili na sio kwa klabu hizo.
Mourinho aliendelea kumtupia Conte maneno siku ya Jumamosi kwa kusema yeye hawezi "kupigwa marufuku yoyote kwa kosa la kupanga matokeo ya mechi", ambapo awali alikuwa amezungumzia kuhusu "mchekeshaji" uwanjani.
Mwitaliano huyo alijibu matamshi ya Mourinho kwa kumuita mtu ''mdogo.''
"Alitumia maneno makali,'' Conte aliongeza kwenye mkutano wake na wanahabari siku ya Junanne.
''Sitasahau hili.''
Conte amesema hajutii kusema ''Huyu ni mtu mdogo'' kwenye matamshi yake na hakuna sababu yoyote kwa Chama cha Mameneja wa Ligi ya Premia kuingilia kati.
"Hii si shida kutoka kwa klabu, ni shida kati yetu sisi. Nimenyamaza,'' aliongeza.
RAIS wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), Wallace Karia ametuma salamu za rambirambi kufuatia kifo cha beki wa zamani wa kimataifa wa Tanzania, Omary Kapera aliyefariki dunia juzi kuzikwa jana mchana. Rais Karia amesema kwamba amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za msiba huo; "Nimeshtushwa na taarifa hizo za kifo cha Kapera hasa ikichukuliwa bado tupo kwenye majonzi ya kumpoteza mchezaji mwingine wa zamani Athuman Juma Chama, kwa niaba ya Shirikisho natoa pole kwa wote walioguswa na msiba huo kuanzia kwa familia, ndugu, jamaa na marafiki,”alisema Rais Karia. Omar Kapera ‘Mwamba Kifua’ alikuwa sentahafu wa Yanga tangu miaka ya 1960 hadi 1977 alipokwenda kujiunga na Nyota Afrika ya Morogoro kufuatia mgogoro mkubwa uliobuka klabu ya Jangwani mwaka 1976. Kapera na kundi la wachezaji wenzake walioondoka Yanga baada ya mgogoro huo wa kihistoria, baadaye walirejea Dar es Salaam kuasisi Pan Africans iliyokuja kuwa tishio pia katika soka ya Tanzania kabla ya kupoteza makali baada ya muongo mmoja. Kapera alikuwepo kwenye kikosi cha Yanga kilichoichapa Simba SC 5-0 Juni 1, mwaka 1968 Uwanja wa Karume, Dar es Salaam siku hiyo mabao ya wana Jangwani yakifungwa na Maulid Dilunga mawili dakika ya 18 kwa penalti na 43, Salehe Zimbwe dakika za 54 na 89 na Kitwana Manara ‘Popat’ dakika ya 86. Na ni kikosi hicho kilichofika Robo Fainali ya Ligi ya Mabingwa Afrika mara mbili mfululizo mwaka 1969 na 1970 na kutolewa na Asante Kotoko ya Ghana mara zote.
Ukisema
kuwa amewanyamazisha pia ni sawa maana Joh Raphael Bocco amekuwa
akionyesha kiwango bora dhidi ya wale waliokuwa wakiamini kuwa hana
msaada.
Kiwango
anachoendelea kukionyesha mshambuliaji, John Bocco kimetosha kwa Kaimu
Kocha Mkuu wa Simba Mrundi, Masoud Djuma kumpa unahodha mkuu nyota huyo.
Hiyo,
ikiwa ni siku chache tangu mshambuliaji huyo aifungie mabao muhimu
katika mechi dhidi ya Ndanda FC iliyochezwa wikiendi iliyopita kwenye
Uwanja wa Nangwanda Sijaona, Mtwara na matokeo kumalizika kwa Simba
kushinda mabao 2-0.
Bocco
anapewa cheo hicho cha nahodha mkuu akimrithi beki Mzimbabwe, Method
Mwanjali aliyesitishiwa mkataba wake katika usajili wa dirisha dogo
ambalo lilifungwa Desemba 15, mwaka huu.
Djuma
alisema awali kabla ya kumpa cheo hicho, alikuwa ni nahodha msaidizi wa
timu hiyo akisaidiana na beki wa kushoto, Hussein Mohamed ‘Zimbwe Jr’.
Djuma
alisema anafurahishwa na kiwango cha Bocco anayecheza vizuri kwa
kufuata maelekezo yake ambayo anampa kabla na baada ya mechi katika
kuhakikisha anatimiza majukumu ya kufunga mabao.
“Nimempa
cheo hicho cha unahodha mkuu kutokana na nidhamu yake ya ndani na nje
ya uwanja, pia jinsi anavyotimiza majukumu yake akiwa uwanjani kwa maana
kufunga mabao na kiwango kizuri anachokionyesha,” alisema Djuma.
Nyota wa timu ya Liverpool ambaye ni
raia wa Misri, Mohamed Salah ametangazwa mshindi wa tuzo ya mchezaji
bora wa Afrika wa mwaka 2017 Shirikisho la soka barani Afrika (CAF).
Salah
alikuwa akishindana na Pierre-Emerick Aubameyang, na Sadio Mane na
akaibuka bora zaidi kwa wingi wa kura na ubora awapo kiwanjani. Mane
na Salah walihudhuria sherehe za kutangazwa kwa washindi mjini Accra,
Ghana saa 24 kabla ya mechi ya Kombe la FA Ijumaa ambapo klabu yao ya
Liverpool itacheza dhidi ya Everton. Salah hataweza kucheza mechi hiyo kwani ameumia.
Salah ametwaa tuzo hiyo kwa mara ya kwanza maishani mwake. Salah
alionekana kuitetea vyema timu yake ya Liverpool mwaka 2017 baada ya
kujipatia goli 23 katika mechi 29 baada ya kujiunga katika ligi kuu ya
England akitokea timu ya AS Roma.
Mchezaji nyota wa tenisi duniani Serena Williams amejiondoa kutoka kwa michuano ya mwezi huu ya Australian Open mjini Melbourne.
Mmarekani huyo wa miaka 36 alicheza mechi yake ya kwanza wiki iliyopita tangu ajifungue Septemba.
Williams,
ambaye ameshinda Grand Slam mara 23 na ndiye bingwa mtetezi wa
Australian Open alisema: "Ingawa nakaribia sana, sijafika pahali
ninapotaka."
Alhamisi, Mwingereza Andy Murray pia alijiondoa kutoka kwa michuano hiyo itakayoanza 15 Januari.
William alikuwa na ujauzito wa wiki sita wa binti yake Olympia aliposhinda taji lake la saba la Australian Open mwaka 2017. Serena
Williams ambaye kwa sasa ameorodheshwa nambari 22 duniani alisema:
"Mkufunzi wangu na maafisa wangu husema mara kwa mara kwamba unafaa
kwenda kwa mashindano iwapo uko tayari kushindana hadi mwisho
Kuna uwezekano mkubwa kwamba
Liverpool watamruhusu Philippe Coutinho, 25, kuhamia Barcelona mwezi huu
wa Januari kwa £140m. (Times)
Chelsea wanamtaka meneja wa
Atletico Madrid Diego Simeone achukue nafasi ya Antonio Conte katika
klabu hiyo mwisho wa msimu. (Times )
Chelsea wamezidisha juhudi
zao za kutaka kumnunua kiungo wa kati wa Everton na England Ross
Barkley, 24, na pia wameulizia kuhusu uwezekano wa kumnunua mshambuliaji
wa England na West Ham Andy Carroll, 28. (Mail)
Mchezaji wa Celtic na Scotland Kieran Tierney, 20, amejumuishwa
katika orodha ya mabeki wa kushoto ambao Manchester United wanawatafuta
kuimarisha safu yao ya ulinzi, pamoja na kinda wa Fulham Ryan Sessegnon,
17. (Daily Record)
Paris St Germain wanatarajiwa kutoa ushindani
kwa Tottenham katika kutafuta saini ya Sessegnon ambaye thamani yake
imekadiriwa kuwa £30m. (Mirror)
Juventus wana imani kwamba watafanikiwa kumchukua Emre Can kutoka Liverpool bila kulipa ada yoyote mwisho wa msimu.
Klabu hiyo ya Serie A imemuahidi mchezaji huyo wa miaka 23 mshahara wa £85,000 kwa wiki. (Guardian)
Manchester
United wameanzisha mazungumzo ya kuongeza mikataba ya wachezaji wane
kwa mwaka mmoja. Wachezaji hao ni viungo wa kati wa Uhispania Juan Mata,
29, na Ander Herrera, 28, beki wa England Ashley Young, 32, na beki
Mholanzi Daley Blind, 27. (Mirror)
Manchester United wanataka sana
kumnunua beki wa kushoto wa Juventus Sandro lakini wanavunjwa moyo na
Juve kutotaka kumuuza mchezaji huyo wa miaka 26. (Express)
Tottenham
wanatarajiwa kutoa mikataba mipya yenye donge nono zaidi kwa
mshambuliaji wa England Harry Kane, 24, na beki wa Ubelgiji Toby
Alderweireld, 28. (Independent)
Marseille wanamnyatia kiungo wa
kati wa Arsenal Jack Wilshere lakini mchezaji huyo wa miaka 26 anataka
kusalia na Gunners. (Mail)
Mkufunzi mkuu wa Monaco Leonardo Jardim amesema hana
nia ya kumuuza mshambuliaji wake Mfaransa Thomas Lemar, 22, kwa
Liverpool mwezi huu. (Liverpool Echo)
Meneja wa Paris St-Germain
Unai Emery amefungua mlango kwa winga wa Brazil Lucas Moura, 25, na
mwenzake wa Ufaransa Hatem Ben Arfa, 30, kuihama klabu hiyo Januari.
(L'Equipe)
Mbelgiji Thibaut Courtois, 25, anakaribia kutia saini mkataba
mpya Chelsea baada ya klabu hiyo kumpa ujira wa zaidi ya £200,000 kwa
wiki, hatua itakayomfanya kuwa kipa anayelipwa pesa nyingi zaidi
duniani. (Telegraph)
Beki wa Chelsea David Luiz, 30, anataka sana
kuondoka klabu hiyo na anatumaini Real Madrid watamtaka. (Mundo
Deportivo - kupitia Express)
Mkufunzi mkuu wa Newcastle Rafa
Benitez anatafakari uwezekano wa kutaka kumnunua nahodha wa Watford Troy
Deeney, 29. (Northern Echo)
Newcastle na Burnley nao wanataka kumnunua kiungo wa kati Mhispania Jonathan Viera, 28, kutoka Las Palmas. (Telegraph)
Sunderland wanakaribia kumchukua mshambuliaji mchanga wa Liverpool Ben Woodburn mwenye miaka 18 kwa mkopo. (Star)
Everton wanataka kumnunua kiungo wa kati wa Nice na Ivory Coast Jean Michael Seri, 26. (Sky Sports)
Meneja
wa Everton Sam Allardyce hataki kumwachilia mshambuliaji Sandro
Ramirez, 22, atoke nje kwa mkono Januari lakini anasema hana usemi
wowote kuhusu hilo. (Liverpool Echo)
Crystal Palace wamewasilisha ofay a kutaka kumnunua beki wa kati wa Lille Ibrahim Amadou, 24. (Sun)
Besiktas wanataka kumnunua mshambuliaji wa Leicester na Algeria Islam Slimani, 29. (Leicester Mercury)
Barcelona nao wanakaribia kumchukua beki wa kati wa Palmeiras ambaye ni raia wa Colombia Yerry Mina, 23. (Marca)
Manchester
City nao wamesalia makini sana kutafuta walinzi sokoni kutokana na
mahitaji ya kuwa katika michuano mingi. (Manchester Evening News)
Tamko la Bayern Munich kuhusu kiungo wa kati wa Schalke Leon
Goretzka limekera klabu hiyo, na kuimarisha nafasi ya Liverpool kumnunua
mchezaji huyo wa miaka 22. (Star)
Meneja wa zamani wa Bundesliga
Jos Luhukay ni miongoni mwa wanaopigiwa upatu kuchukua nafasi iliyoachwa
wazi na Carlos Carvalhal klabu ya Sheffield Wednesday. (Yorkshire Post)