Meneja wa Chelsea Antonio Conte amesema 'hatausahau' mzozo ambao alikuwa nao na meneja wa Manchester United, Jose Mourinho akiongeza kwamba hiyo ni shida miongoni mwao hao wawili na sio kwa klabu hizo.
Mourinho aliendelea kumtupia Conte maneno siku ya Jumamosi kwa kusema yeye hawezi "kupigwa marufuku yoyote kwa kosa la kupanga matokeo ya mechi", ambapo awali alikuwa amezungumzia kuhusu "mchekeshaji" uwanjani.
Mwitaliano huyo alijibu matamshi ya Mourinho kwa kumuita mtu ''mdogo.''
"Alitumia maneno makali,'' Conte aliongeza kwenye mkutano wake na wanahabari siku ya Junanne.
''Sitasahau hili.''

Conte amesema hajutii kusema ''Huyu ni mtu mdogo'' kwenye matamshi yake na hakuna sababu yoyote kwa Chama cha Mameneja wa Ligi ya Premia kuingilia kati.
"Hii si shida kutoka kwa klabu, ni shida kati yetu sisi. Nimenyamaza,'' aliongeza.