FC Barcelona walimaliza weekend iliyopita kwa kuongeza wigo wa pointi kwenye La Liga baada ya mechi yao na Villareal.


Barça kwa sasa wana pointi 76, wakati Atletico wana pointi 67, ingawa rekodi ya head to head inalifanya pengo kuwa pointi 10. Timu hizi pia zitakutana katika robo fainali ya michuano ya Kombe la mabingwa wa ulaya.
Real Madrid, wakiwa na pointi 66 baada ya ushindi wao dhidi ya Sevilla jumapili, bado wana nafasi finyu ya kuweka hai matumaini yao kwa ushindi katika mechi ijayo dhidi ya Barca pale Nou Camp, mwezi ujao. Wana pointi 10 nyuma ya vinara, lakini wanaweza kulipunguza kufikia pointi 7 huku ikiwa imebaki michezo 7 ligi kuisha.
Barça-Real Madrid
R. Sociedad-Barça
Barça-Valencia
Deportivo-Barça
Barça-Sporting
Ikiwa Barca atashinda mechi hizo zote, watakuwa wamefikisha pointi 91. Ni idadi ya pointi ambazo Atletico hawawezi kufikia. Atletico wakishinda mechi zao zilizobaki watafikisha pointi 82.
Mechi zao zilizobaki za Atletico
Mechi zao zilizobaki za Atletico
Atletico-Betis
Espanyol-Atletico
Atletico-Granada
Athletic Club-Atletico
Atletico-Rayo V.
Real Madrid pia watashindwa kupata nafasi ya ubingwa ikiwa yatatokea hayo niliyoyaeleza hapo juu.