Social Icons

Pages

Saturday, 24 January 2015

MAAJABU KOMBE LA FA - CHELSEA,MAN CITY,SOUTHAMPTON NA SPURS ZATUPWA NJE.


Maajabu ya kombe la FA pale
England yameendelea kuonekana
baada ya jana Manchester United
United kutoka sare ya bila kufungana
na timu ya daraja la pili ya
Cambridge United leo michezo
kadhaa imepigwa na kushuhudiwa
vigogo wa ligi ya England wakitupwa
nje.

Mechi hizo za Raundi ya nne
zimemalizika muda mfupi uliopita na
kushuhudiwa Vinara wa Ligi Kuu
England Chelsea wakitupwa nje kwa
kufungwa bao 4-2 nyumbani kwao
Stamford Bridge na klabu ya daraja
la Championship Bradford City.

Mabingwa watetezi wa Ligi kuu
Nchini England Manchester City wao
walikubali kichapo cha bao 2-0
nyumbani Etihadi toka kwa
Middlesbrough timu nyingine
inayoshiriki Championship.

Southampton ambao msimu huu
wameonekana wako vizuri na
kushika nafasi ya tatu katika
msimamo wa Ligi walikubali kichapo
cha bao 3-2 toka kwa Crystal Palace
ambayo imeongezwa nguvu kufatia
kumpata kocha mpya Allan Pardew
pambano hilo lilipigwa nyumbani
kwa Southamptob St. Marys
stadium.

Klabu zingine za Ligi kuu ambavyo
vimepata vichapo leo ni pamoja na
Swansea City waliokubali kichapo
cha bao 3-1 toka kwa Blackburn
Rovers ambayo nayo inashiriki Ligi
ya Championship.

Blackburn Rovers
3-1 Swansea

Birmigham City 1-2
West Brom

Cardiff City 1-2
Reading

Chelsea 2-4
Bradford City

Derby County 2-0
Chesterfield

Manchester City 0-2
Middlesbrough

Preston 1-1
Sheffield United

Southampton 2-3
Crystal Palace

Sunderland 0-0
Fulham

Tottenham Hotspurs
1-2 Leicester City
Patrick Blo

 
FULU VIWANJA