Social Icons

Pages

Wednesday, 21 January 2015

AFCON 2015: CAMEROUN NAYO YANUSURIKA KWA MALI!


CAMEROUN-MALIJANA Usiku huko Nuevo Estadio de Malabo, Mjini Malabo katika Mechi ya pili ya Kundi D la Mashindano ya Mataifa ya Afrika, AFCON 2015, Mali na Cameroun zilitoka Sare ya Bao 1-1.

Ambroise Oyongo aliokoa kipigo Cameroun baada ya kusawazisha katika Dakika ya 84 kufuatia Bao la Dakika ya 70 la Mali lilifungwa na Sambou Yatabare.

Mapema Jana kwenye Uwanja huo huo, Ivory Coast na Guinae zilitoka Sare 1-1 katika Mechi ya kwanza ya Kundi D.
 
FULU VIWANJA