Social Icons

Pages

Tuesday, 22 July 2014

Stars bado ina nafasi ya kufuzu”- Mart Nooij

“Stars bado ina nafasi ya kufuzu”- Mart NooijKatika mchezo wa marudiano Stars italazimika kushinda idadi kubwa ya mabao zaidi ili kusonga mbele hatua ya makundi.
KOCHA wa timu ya taifa ya Tanzania ‘Taifa Satrs’Mart Nooij,amesema kikosi chake bado kina nafasi ya kucheza hatua ya makundi katika kuwania kufuzu fainali za mataifa ya Afrika licha ya kulazimishwa sare ya 2-2 na Msumbiji jana.
Nooij ameiambia Goal kwamba matokeo hayo siyo mazuri kwa Stars lakini atahakikisha anazitumia vizuri dakika 90 za Maputo kwa ajili ya kikosi chake kucheza hatua ya Makundi.
“Nikweli sare ya 2-2 nyumbani siyo matokeo mazuri kwetu lakini hatutalala tuta tutahakikisha tunakwenda kupambana Maputo na kupata ushindi kama tulivyo fanya Harare kwenye mechi yetu na Zimbabwe.
Katika mchezo wa marudiano Stars italazimika kushinda idadi kubwa ya mabao zaidi ili kusonga mbele hatua ya makundi.
 
FULU VIWANJA