
Nooij ameiambia Goal kwamba matokeo hayo siyo mazuri kwa Stars lakini atahakikisha anazitumia vizuri dakika 90 za Maputo kwa ajili ya kikosi chake kucheza hatua ya Makundi.
“Nikweli sare ya 2-2 nyumbani siyo matokeo mazuri kwetu lakini hatutalala tuta tutahakikisha tunakwenda kupambana Maputo na kupata ushindi kama tulivyo fanya Harare kwenye mechi yetu na Zimbabwe.
Katika mchezo wa marudiano Stars italazimika kushinda idadi kubwa ya mabao zaidi ili kusonga mbele hatua ya makundi.