
Nkamia alisema Jeshi hilo limekuwa na timu zisizopungua tano kwenye ligi kuu ya Tanzania bara inayoshirikisha timu 14 lakini ni timu mbili peke zinazo mudu ushindani kwenye ligi hiyo zilizobaki zimekuwa kama wasindikizaji jambo ambalo ameliita ni sawa na ubadhilifu wafedha.
“Itapendeza kuona kama TFF,itaketi na wenzetu wa Jeshi la JKT,na kuweka mikakati ya kuwa na angalau timu mbili kwenye ligi kuu ambazo zitaandaliwa vizuri na kutoa ushindani wa kweli kwenye ligi tofauti na hivi sasa ambapo jeshi hilo lina timu tano ni zote hazina mwenendo mzuri kwenye ligi.
Timu za Jeshi ambazo zilishiriki ligi kuu msimu uliopita ni JKT Ruvu,Ruvu Shooting,Mgambo JKT,Rhino Rangars na JKT Oljoro kati ya hizo mbili za Oljro na Rhino zimeshuka daraja huku Mgambo ya Kabuku Tanga ikiponea chupuchupu kushuka daraja.