Social Icons

Pages

Friday, 25 July 2014

LA LIGA: RATIBA MSIMU MPYA YATOKA, SUAREZ KUMALIZIA KIFUNGO ‘EL CLASICO’!



RFEF, Shirikisho la Soka Spain, Leo limetangaza Ratiba ya La Liga kwa Msimu mpya wa 2014/15 na Vigogo, Real Madrid watakuwa Wenyeji wa Barcelona hapo Oktoba 26 kwenye Mechi ambayo huenda ikawa ya kwanza kwa Luis Suarez kwa Timu yake Barca baada ya kumaliza Kifungo chake cha Miezi Minne.
SUAREZ-IN-BARCALigi hiyo itaanza Wikiendi ya Agosti 23 na Mabingwa Watetezi, Atletico Madrid, wataanza na Rayo Vallecano.
Real Madrid na Barcelona zote zitaanzia Nyumbani kwa Real kucheza na Cordoba na Barca kuivaa Elche.
Kwenye Ratiba ya ufunguzi, Sevilla watakuwa Nyumbani kucheza na Valencia ikiwa ni kama Marudiano ya Fainali ya EUROPA LIGI ya Msimu uliopita.
Pia Wikiendi hiyo itakuwepo Dabi ya Jiji la Vila-real kati ya Levante na Villareal wakati Malaga wataanza na Athletic Bilbao ndani ya La Rosaleda.
Mechi ya Marudiano ya El Clasico itakuwa huko Camp Nou wakati Barcelona watakapoikaribisha Real hapo Machi 22, 2015.
LA LIGA
Mechi za Ufunguzi Msimu mpya 2014/15
Wikiendi Agosti 23-24
Sevilla-Valencia
Barcelona-Elche
Rayo Vallecano-Atlético de Madrid
Eibar-Real Sociedad
Real Madrid-Córdoba
Celta-Getafe
Levante-Villarreal
Málaga-Athletic Club
Almería-Espanyol
Granada-Deportivo

 
FULU VIWANJA