ATLETICO MADRID ndio Vinara wapya wa La
Liga baada kuichapa Real Sociedad Bao 4-0 huku Real Madrid wakitoka Sare
na Athletic Bilbao na Cristiano Ronaldo kutolewa nje kwa Kadi Nyekundu
ya utata.
Atletico walifunga Bao zao kupitia David Villa, Diego Costa, Miranda na Diego Ribas.
Ushindi huo umeifanya Atletico iongoze
Ligi kwa mara ya kwanza tangu 1996 na wapo Pointi 3 mbele ya Barcelona
na Real Madrid ambao wamefungana kwa Pointi.
MSIMAMO-Timu za Juu:
|
NA |
TIMU |
P |
W |
D |
L |
F |
A |
GD |
PTS |
|
1 |
Atletico de Madrid |
22 |
18 |
3 |
1 |
56 |
14 |
42 |
57 |
|
2 |
FC Barcelona |
22 |
17 |
3 |
2 |
59 |
16 |
43 |
54 |
|
3 |
Real Madrid CF |
22 |
17 |
3 |
2 |
61 |
22 |
39 |
54 |
|
4 |
Athletic de Bilbao |
22 |
13 |
4 |
5 |
42 |
28 |
14 |
43 |
Nao
Real Madrid, wakicheza Ugenini, walishindwa kuipiku Barca na kukamata
Nafasi ya Pili baada kutoka Sare 1-1 na Athletic Bilbao.
Real walitangulia kufunga kwa Bao la
Jese Rodriguez katika Dakika ya 64 na Bilbao kusawazisha kupitia Ibai
Gomez Dakika 10 baadae.
Ndipo ilipotokea rabsha Golini na
Ronaldo kupewa Kadi Nyekundu wakati marudio yalionyesha hakufanya kosa
lililostahili Kadi hiyo.