Social Icons

Pages

Sunday, 2 February 2014

MAN CITY v CHELSEA: MTANANGE JUMATATU USIKU

!

MOURINHO.MSTARINI_MIKONO_JUUJUMATATU Usiku, Etihad, itazikutanisha Manchester City na Chelsea ambazo zinaifukuza Arsenal iliyo kileleni mwa Ligi Kuu England na umuhimu wa Mechi hii haujapotea kwa Jose Mourinho, Meneja wa Chelsea, ambae Siku zote yuko tayari kutumia mbinu yeyote ili kuzua hofu na kuwapoteza Wapinzani wake.
Safari hii, Mourinho ameipania Man City, ambao pamoja na Arsenal, ndio wanaonekana ni tishio kwake katika mbio za Ubingwa Msimu huu.

LIGI KUU ENGLAND
MSIMAMO-Timu za Juu:
NA
TIMU
P
GD
PTS
1
Arsenal
24
26
55
2
Man City
23
42
53
3
Chelsea
23
23
50
4
Liverpool
24
29
47
5
Everton
24
12
45
6
Tottenham
24
-1
44
7
Man Utd
24
10
40
+++++++++++++++++++++++++++
Akiongea na Wanahabari kuelekea mpambano wao muhimu, Mourinho aliiponda Man City na kudai haijafanya lolote la maana tangu inunuliwe na Tajiri toka Falme za Nchi za Kiarabu, Sheikh Mansour, Mwaka 2008 ukilinganisha na Fedha alizotumia.
Tangu wakati huo, Man City imetwaa FA CUP Mwaka 2011, Ligi Kuu England Mwaka 2012 lakini kwenye UEFA CHAMPIONZ LIGI ni Msimu huu tu wamefika Raundi ya Mtoano ya Timu 16 baada ya kutupwa nje mara mbili kwenye Hatua za Makundi na hata safari hii wana kimbembe kwani Mpinzani wao ni Barcelona ambae watacheza nae Mechi ya Kwanza Etihad Februari 18.
Mourinho amesema: “Wametwaa Ubingwa mara moja, Vikombe viwili. Timu yao nzuri na wanatakiwa kushinda Mataji mengi zaidi!”
Wamiliki hao wa Man City, tangu Mwaka 2008 wametumia zaidi ya Pauni Milioni 700 kununua Wachezaji.
Lakini Mourinho amepinga kauli ya Meneja wa Tottenham, Tim Sherwood, ambae alidai Man City ndio Timu Bora Duniani mara baada ya Juzi kutwangwa Bao 5-1 na City, Spurs walipokuwa Uwanjani kwao White Hart Lane.
Mourinho amedai City wana bahati na pia kusaidiwa na Marefa.
+++++++++++++++++++++++++++
Man City==Bahati yao ya Mtende:
26 Desemba: Ushindi wao 2-1 na Liverpool
- Raheem Sterling alifunga Bao safi kuipa uongozi Liverpool na Refa akaamua Ofsaidi
- Luis Suarez alivutwa Jezi waziwazi na Joleon Lescott Dakika za mwishoni na Refa kupeta.
12 January: Ushindi wao 2-0 na Newcastle
- Cheick Tiote alifyatua mzinga wa Mita 25 na kutinga wavuni lakini Refa akaamua Yoan Gouffran alikuwa Ofsaidi licha ya kutohusika chochote.
29 January: Ushindi wao 5-1 na Tottenham
- Wakiwa nyuma kwa Bao 1-0, Spurs walisawazisha kwa Bao safi la Michael Dawson lakini likakataliwa kwa Ofsaidi.
- Danny Rose, Beki wa Spurs, alitolewa nje kwa Kadi Nyekundu licha ya kuucheza Mpira ikidaiwa alimchezea Rafu Edin Dzeko na kutolewa Penati iliyowapa City Bao la pili na kuongoza 2-0.

Akipasua ukweli wake, Mourinho ametamka: “Maumuzi mengi muhimu yamekwenda upande wao. Wana bahati. Marefa wanajitahidi na na mara nyingne wanafanya makosa na kawaida makosa hayo hugawanyika kwa kila Timu. Lakini kwao, kila kitu kipo upande wao.”
Hata hivyo, Meneja wa Man City, Manuel Pellegrini, alikataa kuvutwa katika mzozo na Mourinho na kudai: “Hii si Mimi dhidi ya Mourinho au yeye na Mimi! Jumatatu ni Manchester City dhidi ya Chelsea, Timu zote zinagombea Ubingwa.”
Kwenye Mechi hii, Man City itamkosa Straika wao mahiri Sergio Aguero, ambae Msimu huu ameshafunga Bao 26, alieumia Musuli ya Pajani [Hamstring] walipoifunga Tottenham.
Man City wameshinda Mechi zao zote 11 za Ligi walizocheza Uwanjani kwao Etihad Msimu huu wakipiga wastani wa Bao 4 kila Mechi na tayari washabamiza Jumla ya Mabao 115 katika Mechi zao zote za Msimu huu.
 
FULU VIWANJA