Social Icons

Pages

Tuesday, 24 December 2013

‘PIGA UA’ ALHAMISI, BOKSING DEI HUKO ETIHAD,liverpool dhidi ya man city


NI WAZI Msimu huu Timu za Ligi Kuu England huwa zinagwaya kwenda Etihad kupambana naManchester City ambako katika Mechi zao 8 za Ligi wameshinda zote kwa Jumla ya Bao 35.
Miongoni mwa Mechi hizo 8, City, walio chini ya Meneja Manuel Pellegrini, imeshusha vipigo kwa Mabingwa Watetezi Man United Bao 4-1, Tottenham 5-0 na Arsenal 6-3.
Lakini, safari hii, wageni wa City ni Liverpool ambao wanaongoza Ligi katika Kipindi hiki cha Krismasi kwa mara ya kwanza tangu Msimu wa 2008/09 na wanae Straika bora kwa sasa Luis Suarez ambae ndie Mfungaji Bora akiwa na Bao 19.

JE WAJUA?
-Liverpool wameshindwa kuwa Bingwa katika mara zote tatu za mwisho walizoongoza Ligi wakati wa Krismasi.
-Mara hizo 3 ni 1990-91 walipomaliza Nafasi ya 2, Mwaka 1996-97 walipomaliza Nafasi ya 4 na 2008/09 walipomaliza Nafasi ya 2 nyuma ya Man United.

Hata hivyo, Liverpool wakiwa Ugenini ni nyanya kidogo na katika Mechi zao 8 za Ligi za Ugenini wamefungwa Bao 13
Wachambuzi wengi walikuwa na hamu na Mechi hii kuwaona Mastraika wanaong’ara Sergio Arguero wa City na Luis Suarez wakipambana uso kwa uso lakini, kwa bahati mbaya, Aguero hatakuwepo kwa vile ni Majeruhi na badala yake City wanaweza kumchezesha Alvaro Negredo au Edin Dzeko.

-Mechi 6 kati ya 9 zilizopita za Ligi kati ya City na Liverpool zilimalizika kwa Sare huku City wakishinda 2 na Liverpool 1 Uwanjani kwao Anfield kwa Bao 3-0.

Lakini nguzo kubwa ya Timu ya City ni Kiungo chao hatari ambacho Msimu huu kimeimarika baada kumpata Fernandinho ambae ameonyesha ushirikiano mzuri sana na Yaya Toure kiasi cha kuwaruhusu David Silva na Jesus Navas kuwa huru kutiririka na Soka lao lenye akili ambalo huzichanganya ngome nyingi na kutoa mwanya wa Goli nyingi.
Kwa kawaida kukosekana kwa Mkongwe na Nahodha wa Liverpool, Steven Gerrard, kungekuwa pigo kubwa kwa Liverpool lakini katika Mechi za hivi karibuni kutokuwepo kwake kwa sababu ya maumivu kumefungua njia kwa Liverpool kutumia Viungo Chipukizi, kina Allen, Lucas, Henderson, Coutinho na Sterling,   wanaokwenda mbio mithili ya umeme na kumlainishia umaliziaji Luis Suarez.
 
FULU VIWANJA