Social Icons

Pages

Tuesday, 24 December 2013

LUKAKU AKANA KUWA NA BIFU NA MOURINHO

Romelu Lukaku amesisitiza kuwa hana matatizo yeyote na Meneja wa Chelsea Jose Mourinho.
Lukaku, mwenye Miaka 20, ambae yupo kwa Mkopo Everton tangu mwanzoni mwa Msimu huu akitokea Chelsea, amekanusha habari zilizozagaa kuwa kutuwa kwake huko Goodison Park ni kutokana na bifu na Mourinho.
Akiwa na Everton, Lukaku, ambae pia huchezea Timu ya Taifa ya Belgium, amefunga Bao 8 katika Mechi 13.
Lukaku ameeleza kuhamia kwake kwa Mkopo huko Everton ni matakwa yake yeye mwenyewe ili apate nafasi ya kucheza mara kwa mara ili ajiendeleze zaidi baada ya Msimu uliopita pia kucheza kwa Mkopo huko West Brom.
Akiongea na Jarida la Sport Voetbal, Lukaku alieleza: “Mwanzoni nilisema nataka kubaki Chelsea. Lakini baadae niliona bora niondoke ili nipate nafasi zaidi ya kucheza. Ni lengo langu kufanya vizuri zaidi kupita Msimu uliopita. Nataka ni we mmoja wa Mastraika bora Duniani. Natumai naweza kuwekwa sawa na Cavani, Ibrahimovic, Van Persie, Suarez na Lewandowski katika Miaka miwili ijayo.”
Aliongeza: “Nimekuwa na Jose Mourinho kwa Miezi miwili. Hatukuwa na tatizo. Yeye allitaka nibaki na aliniuliza kwanini nataka kuondoka!”
Pia Lukaku alihakikisha kuwa atarudi tena Chelsea na ndio maana alisaini Mkataba wa Miaka mitanowww.fulu viwanja blogsop .com
 
FULU VIWANJA