Social Icons

Pages

Monday, 16 December 2013

COPA del REY: RONALDO KURUDI KUIKOMOA 'TIMU NDOGO' XATIVA ILIYOWABANA?




RONALDO-FURAHACOPA del REY, Kombe la Mfalme huko Spain, leo lipo kwenye Mechi za Marudiano za Raundi ya Mtoano ya Timu 32 na Mabingwa wa Spain, Barcelona wako kwao Nou Camp kurudiana na Timu ya Daraja la chini, FC Cartagena, ambayo waliitwanga 4-1 Wiki mbili zilizopita.
Mabingwa Watetezi wa Copa del Rey, Atletico Madrid, wako kwao Estadio Vicente Calderon, kurudiana na Sant Andreu, pia ya Daraja la chini, ambayo waliifunga 4-0.
Lakini, macho yote yatakuwa huko Santiago Bernabeu, ambako Vigogo, Real Madrid, wanarudiana na Timu ndogo, Olimpic Xativa, waliyotoka nayo 0-0 katika Mechi ya Kwanza ambayo walicheza bila Cristiano Ronaldo aliekuwa Kifungoni kufuatia Kadi Nyekundu aliyopewa kwenye Fainali ya Kombe hili Msimu uliopita Real walipofungwa 2-1 na Atletico Madrid.
 
FULU VIWANJA