Social Icons

Pages

Monday, 2 February 2015

FA CUP: JUMANNE MAN UNITED KURUDIANA NA CAMBRIDGE UNITED OLD TRAFORD

VIGOGO wa England,
Manchester United, ambao wao
pamoja na Mabingwa Watetezi
Arsenal, ndio wanashika
Rekodi ya kutwaa FA CUP mara
nyingi, mara 11 kila mmoja ,
Jumanne Usiku wanarudiana
na Cambridge United Uwanjani
Old Trafford baada ya kutoka
0 -0 katika Mechi ya kwanza
iliyochezwa Abbey Stadium
Nyumbani kwa Timu hiyo ya
Daraja la Chini , Ligi 2 .

Hii ni Mechi ya Raundi ya 4 ya
FA CUP na Mshindi atatinga
Raundi ya 5 na kucheza na
Mshindi kati ya Preston au
Sheffield United ambao nao
wanarudiana Jumanne .

Mara ya mwisho na pekee kwa
Cambridge United kucheza
Uwanjani Old Trafford ni
Mwaka 1991 walipotwangwa
Bao 3 - 0 kwenye Kombe la Ligi
ambalo sasa linaitwa Capital
One Cup.

 
FULU VIWANJA