Social Icons

Pages

Tuesday, 27 January 2015

CHELSEA WASHINDA DAKIKA ZA JIONI.NAKUWATOA LIVERPOOL

Mechi ya Marudiano ya Nusu
Fainali ya Capital One Cup
Uwanjani Stamford Bridge kati
ya Chelsea na Liverpool ilienda
Dakika 120 baada ya kuwa
Sare 0 -0 katika Dakika 90 na
Chelsea kushinda Bao 1 -0
katika Dakika za Nyongeza 30.

Ingawa Chelsea walipata Sare
ya 1- 1 huko Anfield Wiki
iliyopita na kikawaida
wangeshinda kwa Goli la
Ugenini, Mashindano haya
hayahesabu Magoli ya Ugenini
kuwa Mawili hadi baada ya
Mechi kumaliza Dakika 120 .

Hata hivyo , Dakika ya 4 tu
baada ya Dakika za Nyongeza
30 kuanza , Frikiki ya Willian
iliunganishwa vizuri kwa
Kichwa na Baranislav Ivanovic
na kuwapa Chelsea Bao moja
na la ushindi .

Leo Jumatano ni Marudiano ya
Nusu Fainali nyingine kati ya
Sheffield United na Tottenham
Nyumbani kwa Sheffield .

Katika Mechi ya kwanza
iliyochezwa pia Wiki iliyopita
huko White Hart Lane,
Tottenham iliifunga Sheffield
United Bao 1 -0 kwa Bao la
Penati iliyotolewa Dakika ya
75 baada ya Jay McEveley
kuushika Mpira na Andros
Townsend kupiga Penati hiyo
na kufunga.

 
FULU VIWANJA