Social Icons

Pages

Thursday, 3 April 2014

MACARI: ‘IKIWA WENGER YUPO ARSENAL MIAKA 9 BILA KOMBE, MOYES MIEZI 9 TU

MOYES-OLD_TRAFFORD_TOUCHLINEMCHEZAJI wa zamani wa Manchester United Lou Macari amemtetea Meneja wa Klabu hiyo, David Moyes, ambae anasakamwa kufuatia kusuasua kwa Mabingwa hao Msimu huu.
Man United, ambao ndio Mabingwa Watetezi wa Ligi Kuu England, hawana nafasi tena kuutetea Ubingwa wao Msimu huu ambao ni wa kwanza kwa Moyes kwani wapo Nafasi ya 7 na wapo Pointi 10 nyuma ya ya zile Timu 4 Bora.
Hali hii iliwafanya baadhi ya Mashabiki wa Man United kukodi Ndege na kuirusha juu ya Old Trafford Jumamosi walipocheza na Aston Villa huku ikivuta Bango kubwa: “WRONG ONE, MOYES OUT”
Macari amesema: “Ni sahihi kusema mambo si mazuri Old Trafford hivi sasa. Lakini Moyes apewe muda hata kama Ndege nyingi zitaruka juu ya Old Trafford!”
Akitetea kuwa Moyes anahitaji muda kama alivyopewa Sir Alex Ferguson kujenga Timu yake mwenyewe upya.
Alisema: “Ikiwa Meneja wa Arsenal anaweza kwenda Miaka 9 bila Kombe, napenda nifikiri Meneja wa Man United anaweza kukaa Miezi 9 bila Watu kutaka afukuzwe!”
Aliongeza: “Ikiwa Chelsea hawashindi kitu Msimu huu, utamwonaje Mourinho? Je atakuta hali kama hii ya Moyes katika Msimu wake wa kwanza tu? Hakika nataka kuona nini kitatokea ikiwa Arsenal watashindwa kuchukua FA CUP Msimu huu!”
 
FULU VIWANJA