Social Icons

Pages

Thursday, 27 February 2014

SHAW, STERLING, BARKLEY WAPO ENGLAND!!


MENEJA WA ENGLAND, Roy Hodgson, amewaita Wachezaji 30 kwa ajili ya Mechi ya Kirafiki ya Jumatano ijayo dhidi ya Denmark Uwanjani Wembley.
Mechi hii ndio ya mwisho ya England kabla Hodgson hajateua Kikosi chake kwa ajili ya Fainali za Kombe la Dunia zitazoanza Juni 12 huko Brazil.
Miongoni mwa Wachezaji walioitwa ni Fulbeki wa Kushoto wa Southampton, Luke Shaw, mwenye Miaka 18, ambae hii ni mara yake ya kwanza kuitwa.
Pia wamo Winga wa Liverpool Raheem Sterling, Miaka 19, na Kiungo wa Everton Ross Barkley, Miaka 20.
Vile vile yupo Sentahafu wa Cardiff City, Steven Caulker, Miaka 22, ambae ni mara yake ya kwanza kuitwa baada ya Mwaka mmoja na katika Mechi pekee aliyoichezea England ni ile ya Novemba 2012 ambayo alifunga Bao lakini England ilichapwa na Sweden kwa Bao 4 za Zlatan Ibrahimovic.
KIKOSI KAMILI:
MAKIPA: Fraser Forster (Celtic), Ben Foster (West Bromwich Albion), Joe Hart (Manchester City), John Ruddy (Norwich City).
MABEKI: Leighton Baines (Everton), Gary Cahill (Chelsea), Steven Caulker (Cardiff City), Ashley Cole (Chelsea), Glen Johnson (Liverpool), Luke Shaw (Southampton), Chris Smalling (Manchester United), Kyle Walker (Tottenham Hotspur).
VIUNGO: Ross Barkley (Everton), Michael Carrick (Manchester United), Tom Cleverley (Manchester United), Steven Gerrard (Liverpool), Jordan Henderson (Liverpool), Adam Lallana (Southampton), Frank Lampard (Chelsea), James Milner (Manchester City), Alex Oxlade-Chamberlain (Arsenal), Raheem Sterling (Liverpool), Andros Townsend (Tottenham Hotspur), Jack Wilshere (Arsenal).
MAFOWADI: Jermain Defoe (Toronto FC), Rickie Lambert (Southampton), Jay Rodriguez (Southampton), Wayne Rooney (Manchester United), Daniel Sturridge (Liverpool), Daniel Welbeck (Manchester United).
 
FULU VIWANJA