Social Icons

Pages

Saturday, 8 March 2014

FA CUP-ROBO FAINALI: LEO ARSENAL KUIVAA EVERTON!!



FA_CUP_2013-2014
Arsenal watacheza bila Kiungo Jack Wilshere ambae alivunjika Mguu kwenye Mechi ya England na Denmark Juzi Jumatano.
Meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, amegusia kuwa Sentahafu Laurent Koscielny yuko fiti lakini Aaron Ramsey na Kim Kallstrom bado ni Majeruhi.
Nahodha wa Everton, Phil Jagielka, ana hatihati kubwa ya kucheza akikabiliwa na tatizo la Musuli za Pajani [Hamstring] lakini Beki mwenzake, Antolin Alcaraz, yuko tayari kurejea baada kuwa nje Gemu 6 akikabiliwa na tatizo la Musuli.

Arsenal walifungwa 1-0 na Stoke City Wikiendi iliyopita kwenye Mechi ya Ligi Kuu England lakini Wenger anategemea Timu yake kuibuka na ushindi ili waendelee kwenye mbio za kutwaa Kombe lao la kwanza tangu Mwaka 2005.
Wenger amesema: “FA CUP ni moja ya vitu muhimu kwetu! Tulihuzunishwa kufungwa na Stoke na ni muhimu kushinda Mechi hii!”
Nae Meneja wa Everton Roberto Martinez, ambae Timu yake ilitoka Sare ya 1-1 na Arsenal kwenye Ligi Mwezi Desemba Uwanjani Emirates, anaamini Timu yake ipo kwenye wakati mbaya kucheza na Arsenal wakati huu.
Amesema: “Itakuwa Gemu ya kusisimua! Wao kucheza Nyumbani ni kitu kikubwa na watajaribu kila kitu kushinda Mechi hii baada ya kufungwa Mechi iliyopita!  Pengine huu ni wakati mbaya kucheza nao!”
 
FULU VIWANJA