MABINGWA YANGA, ambao wamepiga Kambi huko Antalya, Uturuki, leo wamecheza Mechi yao ya
Pili
ya kujipima nguvu na kuichapa Klabu ya Daraja la Pili ya Nchini humo,
Altay SK, Bao 2-0 kwenye Mechi iliyochezwa Viwanja vya Sueno.

Katika Mechi ya Kwanza hapo Juzi, Yanga iliichapa Ankara Sekerspor Bao 3-0.
Hii leo, Yanga ilikuwa na Kocha wao mpya
kutoka Uholanzi, Hans Van Der Plyum, na ilishinda kwa Bao za Didier
Kavumbagu, Dakika ya 46, na Emmanuel Okwi, Dakika ya 57.
Hans Van Der Plyum-Klabu alizofundisha:
-Medeama SC [Ghana]: 16.07.2013 hadi 24.10.2013
-Berekum Chelsea [Ghana]: 01.11.2011 hadi 16.07.2013
-Heart of Lions Kpando [Ghana]: 01.07.2010 hadi 20.09.2011
-Ashanti Gold SC [Ghana]: 01.07.2004 hadi 05.10.2005
-Heart of Lions Kpando [Ghana]: 01.07.2002 hadi 20.07.2003
-Ashanti Gold SC [Ghana]: 01.07.2000) hadi 30.06.2002
-Excelsior Rotterdam [Holland]: 01.07.1995 hadi 30.06.1996
-FC Den Bosch [Holland]: 01.07.1990) hadi 30.06.1995
Yanga, ambayo itakuwa Uturuki kwa Wiki mbili, inatarajiwa kucheza Mechi yake ya Tatu huko Uturuli hivi karibuni.