Social Icons

Pages

Wednesday, 15 January 2014

HIVI NDIVYO MAXIMO ALIVYOWAKATA YANGA



Kocha wa zamani wa Taifa Stars, Marcio Maximo. 

MUDA mfupi baada ya kuingia mkataba wa miezi sita na kocha, Hans Van Der Pluijm, Yanga imetoboa siri kuwa ilishindwa kumpa kazi hiyo kocha wa zamani wa Taifa Stars, Marcio Maximo, aliyetaka alipwe mshahara wa Sh 28.4 Milioni kwa mwezi.
Jana Jumatatu mchana, Yanga ilisaini mkataba wa miezi sita na Van Der Pluijm ambaye ni raia wa Uholanzi. Mara tu aliposaini, kocha huyo aliondoka kwenda Uturuki kujiunga na kikosi kilichopo huko kwa ajili ya maandalizi ya mzunguko wa pili wa Ligi Kuu Bara na mechi za Ligi ya Mabingwa Afrika.
Lakini wakati hilo likitimia, Mwenyekiti wa Kamati ya Usajili ya Yanga, Abdallah Bin Kleb, aliliambia Mwanaspoti kuwa kabla ya kukubaliana na Mholanzi huyo, walizungumza na Mskochi Bobby Williamson wa Gor Mahia ya Kenya ambaye hakuonyesha nia kama alivyofanya Mbelgiji Adel Amrouche wa Harambee Stars, ndipo wakahamia kwa Mbrazili Maximo.
“Maximo alikubali kuja Yanga. Lakini alitaka mshahara mkubwa, dola 18,000 (Sh28 milioni) kwa mwezi. Tukashindwa maana hizo ni fedha nyingi kwetu, viongozi tulijadialiana sana, tukaona hatuwezi kumlipa,” alisema Bin Kleb.
“Unajua fedha za Yanga zinatokana na Wanayanga wenyewe, sasa tusingeweza kuingia mkataba na Maximo halafu tupate tabu ya kumlipa.”
Zaidi ya makocha 50 walielezewa kuomba kazi ya kuwafundisha mabingwa hao wa Tanzania Bara kabla ya klabu hiyo kumalizana na Van Der Pluijm.
Kocha huyo anachukua nafasi ya Mholanzi mwenzake, Ernest Brandts, ambaye alipewa notisi hivi karibuni kutokana na uongozi kueleza kutoridhishwa na kiwango chake. Ilikuwa siku chache baada ya timu hiyo kufungwa na Simba mabao 3-1 katika mechi ya Nani Mtani Jembe.
 
FULU VIWANJA