Social Icons

Pages

Friday, 10 January 2014

TOMAS ROSICKY KUBAKI ARSENAL LAKINI MORATA KUTONASWA!

TOMAS ROSICKY KUBAKI ARSENAL LAKINI MORATA KUTONASWA!
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger amethibitisha kubaki kwa Tomas Rosicky hadi mwishoni mwa Msimu lakini pia amepuuza taarifa zilizozagaa za kumchukua Chipukizi wa Real Madrid, Álvaro Morata, kwa Mkopo.
Rosicky, mwenye Miaka 33 na ambae Mkataba wake unamalizika mwishoni mwa Msimu, amesema yeye anataka kubaki Emirates hadi anastaafu lakini hadi sasa si Wenger wala Klabu iliyothibitisha kumwongezea Mkataba.
Huu ni Msimu wa 8 kwa Rosicky kuwa Arsenal lakini Majeruhi ya mara kwa mara yamemfanya acheze Mechi za Ligi 92 tu.
Wakati huo huo, Wenger amepuuza habari zilizozagaa kuwa Arsenal inataka kumchukua kwa Mkopo Chipukizi wa Real Madrid, Álvaro Morata mwenye Umri wa Miaka 21.
Habari hizi zilishika hatamu mara baada ya Juzi kuthibitishwa kuwa Theo Walcott atakuwa nje Msimu wote uliobaki baada ya kuumia vibaya Goti.
Lakini, hapo Jana, mara baada ya Real Madrid kuifunga Bao 2-0 Osasuna kwenye Mechi ya Copa del Rey ambayo Morata aliingizwa mwishoni kutoka Benchi, Meneja wa Real, Carlo Ancelotti, amesema hana nia ya kumwachia Morata kwenda nje kwa Mkopo.
 
FULU VIWANJA