Social Icons

Pages

Friday, 10 January 2014

ROONEY APELEKWA KWENYE ‘JOTO’, MOYES KUONJA ‘JOTO LA JIWE’ LA FA!



ROONEY_N_MOYES
DAVID MOYES amethibitisha kuwa Straika wake Wayne Rooney amepumzishwa kwa kupelekwa Nchi ya Joto ili kuharakisha kwake kupona Nyonga lakini yeye mwenyewe sasa kuonja ‘Joto la Jiwe’ toka kwa FA ambayo leo imeamua kumfungulia Mashitaka kwa kauli yake: ‘Sasa tunacheza dhidi ya Marefa pamoja na Wapinzani.’
Akithibitisha Rooney na Robin van Persie kukosekana kwa Mechi ya Ligi Kuu England itakayochezwa Jumamosi Old Trafford dhidi ya Swansea City, Meneja wa Manchester United, David Moyes, amesema: “Tumempeleka Rooney kwenye Likizo ya Mazoezi Nchi ya Joto. Atakuwa pamoja na Kocha wa Viungo. Yuko pamoja na Familia yake na tunategemea atakuwa fiti kwa Mechi na Chelsea.”
Man United itasafiri kwenda Stamford Brige Jumapili Januari 19 kucheza Mechi ya Ligi na Chelsea.
Rooney amezikosa Mechi za Man United dhidi ya Swansea na Sunderland na Van Persie hajacheza Mechi tangu Desemba 7, na kabla ya hapo alikuwa hajacheza tangu katikati ya Novemba lakini tangu Alhamisi amerudi kwenye Mazoezi kamili.
WAKATI HUO HUO, David Moyes amefunguliwa Mashitaka na FA, Chama cha Soka cha England, akishitakiwa kwa Utovu wa Nidhamu kufuatia kauli yake mara baada ya kufungwa na Sunderland 2-1 Jumanne iliyopita kwenye Mechi ya Kwanza ya Nusu Fainali ya Capital One Cup alipodai Timu yake sasa ‘inacheza dhidi ya Marefa’ pamoja na Wapinzani.
Baada ya Mechi hiyo, Moyes alidai: “Sasa inabidi tucheze dhidi ya Marefa na Timu pinzani. Ni mbaya sana. Tumeanza kuwacheka. ”
Kilichomkera Moyes ni Refa Andre Marriner kutoashiria Penati lakini aliitoa baada ya ushauri kutoka kwa Mshika Kibendera wake kufuatia Adam Johnson wa Sunderland kuanguka wakati akikabiliana na Tom Cleverley na Moyes kuhoji: “Itakuwaje Mshika Kibendera atoe Penati? Refa alikuwa akiangalia moja kwa moja tukio lile lakini Mshika Kibendera alikuwa haoni kwani kazibwa na Evra! Mchezaji wetu sisi alipewa Kadi kwa tukio kama hilo walilopewa Penati! Hata lile Bao la kwanza ile haikuwa Frikiki ingawa ni kosa letu kutojilinda vizuri kwa Frikiki ile na kuruhusu Bao!”
Moyes amepewa hadi Jumatano Desemba 15 Saa 3 Usiku kujibu Shitaka lake.
Mapema Wiki hii, Meneja wa Liverpool, Brendan Rodgers, alipigwa Faini £8,000 kwa kuhoji kuhusu Refa Lee Mason walipofungwa na Manchester City.
 
FULU VIWANJA