Social Icons

Pages

Wednesday, 15 January 2014

NIKICA JELAVIC AJIUNGA HULL CITY TOKA EVERTON

Everton's striker Nikica Jelavic is pictured at Ewood Park, Blackburn, north-west England on July 27, 2013
Hull City wamekamilisha kumsaini Straika wa Everton Nikica Jelavic kwa Mkataba wa Miaka Mitatu na Nusu.
Jelavic, Raia wa Croatia mwenye Miaka 28, alitaka kuihama Everton ili apate kucheza mara kwa mara ili aongeze nafasi yake ya kuchukuliwa na Nchi yake kwenye Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil Mwezi Juni.
Mwaka huu, Jelavic amefunga Bao 3 tu.
Jelavic alijiunga na Everton Miaka miwili iliyopita akitokea Rangers ya Scotland kwa Dau la Pauni Milioni 5.5 na kuifungia Everton Bao 9 katika Mechi zake 13 za kwanza chini ya Meneja David Moyes.
 
FULU VIWANJA