Social Icons

Pages

Wednesday, 15 January 2014

MOYES AKIRI SHITAKA LA FA

David Moyes Manchester United v Shakhtar Donetsk
David Moyes amekiri Shitaka la FA kufuatia kauli yake mara baada ya kufungwa Bao 2-1 na Sunderland katika Mechi ya Kwanza ya Capital One Cup huko Stadium of Light Wiki moja iliyopita.
Katika Mechi hiyo, Moyes alikasirishwa na Penati waliyopewa Sunderland na kufunga Bao lao la Pili.
Alidai: “Sasa inabidi tucheze dhidi ya Marefa na Timu pinzani. Ni mbaya sana. Tumeanza kuwacheka. ”
Katika Mechi hiyo, Refa Andre Marriner hakuashiria Penati hiyo lakini ilibidi aitoe baada ya ushauri kutoka kwa Mshika Kibendera wake baada Adam Johnson kuanguka wakati akikabiliana na Tom Cleverley.
Kuhusu Sunderland kupewa Penati Jana, Moyes alihoji: “Itakuwaje Mshika Kibendera atoe Penati? Refa alikuwa akiangalia moja kwa moja tukio lile lakini Mshika Kibendera alikuwa haoni kwani kazibwa na Evra! Mchezaji wetu sisi alipewa Kadi kwa tukio kama hilo walilopewa Penati! Hata lile Bao la kwanza ile haikuwa Frikiki ingawa ni kosa letu kutojilinda vizuri kwa Frikiki ile na kuruhusu Bao!”David Moyes Tottenham Hotspur v Manchester United - Premier League
Sasa Moyes atakabiliwa na Faini au Onyo baada ya Kesi yake kusikilizwa na Jopo la Fa huku yeye mwenyewe akikataa kuhudhuria.
 
FULU VIWANJA