Social Icons

Pages

Thursday, 30 January 2014

Kocha atabiri Ronaldo kutamba

KOCHA wa viungo wa timu ya taifa ya Ureno, Antonio Gaspar, amesema anaamini staa wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo atabaki kwenye ubora wake wa sasa kwa miaka sita ijayo.
Ronaldo amedaiwa kuwa na sifa moja ya kujijali na kujiweka sawa muda wote na jambo hilo limemfanya Gaspar kuamini supastaa huyo wa zamani wa Manchester United hatashuka kiwango kwa miaka mingi ijayo. “Kama atataka, Cristiano atabaki kuwa juu kwa miaka mingi ijayo.
Anaweza kuendelea kucheza kwa kiwango bora hata kwenye umri wa miaka 34 au 35 bila ya wasiwasi,” alisema.
Kocha huyo amemtakia mafanikio staa huyo wa Real Madrid ambaye kwa sasa ndiye kinara wa mabao katika Ligi Kuu Hispania, La Liga kutokana kufunga mabao 22.
 
FULU VIWANJA