Social Icons

Pages

Thursday, 30 January 2014

Ligi Kuu yatumia mabilioni usajili 2013

KLABU za Ligi Kuu England zimetumia Pauni 660 milioni kwenye uhamisho wa wachezaji wa kimataifa kwa mwaka jana pekee, huku zaidi ya pauni 50 milioni zikitumika kwenye ada za kulipwa mawakala, imeripoti Fifa.
Klabu za Italia zinafuatia kwa kushika namba mbili kwa kutumia pesa nyingi baada ya kuponda pauni 286 milioni, kisha inakuja Ufaransa (pauni 253milioni), Hispania (pauni 192 milioni) na Ujerumani (pauni 144 milioni).
Nchi ya Brazil imeongoza kuwa na wachezaji wengi waliouzwa ng’ambo, ambapo jumla ni wachezaji 1,558 sawa na asilimia 13.
Klabu za Hispania zimeingiza pesa nyingi zaidi kwenye usajili huo kwa mwaka jana baada ya kuvuna pauni 150 milioni kutokana na kuuza wachezaji wake ng’ambo.
“Kuna klabu chache sana zilizofanya usajili mkubwa ambao ulitetemesha sokoni, lakini usajili mwingine ulikuwa wa kawaida tu,’ alisema Mark Goddard, meneja wa masuala ya uhamisho wa wachezaji Fifa.Kwa England usajili mkubwa wa mchezaji aliyehamia kwenye Ligi Kuu ni ule wa Arsenal walipomnasa Mjerumani Mesut Ozil kwa pauni 42.4 milioni kutoka Real Madrid, wakati uhamisho wa kuuza nje ya nchi ni ule wa Gareth Bale kutoka Tottenham kwenda Madrid kwa pauni 85.3 milioni.
 
FULU VIWANJA