Bausi alilazimika kumuingiza Badru dakika ya 51 kuchukua nafasi ya Khamis
Mcha ‘Vialli’ wa Azam FC, ambaye naye pia amecheza mechi mbili za makundi bila
kufunga.
Hata hivyo, mshambuliaji huyo aliyesajiliwa Simba SC kutoka Canal Suez ya
Misri alishindwa kuinusuru Zanzibar na kipigo cha 2-0 kutoka kwa wenyeji
Harambee Stars.
Angalau kiungo mpya wa Wekundu hao wa Msimbazi, Awadh Juma Issa
aliyesajiliwa kutoka Mtibwa Sugar, alifunga bao zuri la kufutia machozi dhidi
ya Ethiopia, Zanzibar ikilala 3-1.
Kiraka wa Wekundu hao wa Msimbazi, Adeyum Saleh alifunga bao katika ushindi wa 2-1 dhidi ya Sudan Kusini, wakati bao lingine la Zanzibar siku hiyo lilifungwa na kiungo wa Coastal Union, Suleiman Kassim ‘Selembe’.