Me
neja
wa Chelsea Jose Mourinho amekataa kumlaumu Ashley Cole kwa kuhudhuria
Pati ya Krismasi ya Arsenal lakini amethibitisha Beki huyo hana Namba
wakati Chelsea itakapokwenda Emirates kucheza na Arsenal Jumatatu kwenye
Mechi ya Ligi Kuu England.
neja
wa Chelsea Jose Mourinho amekataa kumlaumu Ashley Cole kwa kuhudhuria
Pati ya Krismasi ya Arsenal lakini amethibitisha Beki huyo hana Namba
wakati Chelsea itakapokwenda Emirates kucheza na Arsenal Jumatatu kwenye
Mechi ya Ligi Kuu England.
Cole, Miaka 33, alipigwa Picha akiwa
kwenye Pati ya Arsenal Jumatano ikiwa ni Siku moja tu tokea Chelsea
ifungwe na Sunderland na kutupwa nje ya Capital One Cup.
Mourinho amesema: “Naweka maoni yangu kwangu mwenyewe-ilikuwa ni Siku ya Ofu kwa Wachezaji. Mimi sio Baba, ni Meneja.”
Aliongeza: “Tangu mwanzo, Ashley alikuwa
hachezi. Lakini leo ni Ijumaa, Gemu ipo Jumatatu. Kunaweza kutokea
kitu. Ila nishaamua Branislav Ivanovic ni Fulbeki wa Kulia,
nitamchezesha Cesar Azpilicueta Fulbeki kushoto, nitamchezesha John
Terry na inabidi niamue kati ya Gary Cahill na David Luiz.”
Cole, ambae ni Mchezaji wa Kimataifa wa
England, alicheza Siku ya Jumanne wakati Chelsea inafungwa 2-1 na
Sunderland na kutupwa nje ya Capital One Cup lakini katika Wiki za hivi
karibuni Namba yake imechukuliwa na Cesar Azpilicueta na hajacheza
kwenye Ligi tangu Chelsea ifungwe 2-0 na Newcastle hapo Novemba 2