Social Icons

Pages

Friday, 20 December 2013

CLINT DEMPSEY: FULHAM KUMSAINI TENA

Fowadi wa USA, Clint Dempsey, anatarajiwa kupimwa afya yake Klabuni Fulham ili arejee tenakuchezea Klabuni hapo kwa Mkopo akitokea Seattle Sounders ya USA.
Dempsey, Miaka 30, aliihama Fulham na kujiunga na Tottenham kwa Dau la Pauni Milioni 6 Mwaka 2012 na kisha kuhamia Seattle Sounders Mwezi Agosti Mwaka huu.
Mkopo huu utamsaidia Dempsey kuendelea kucheza hadi Msimu mpya wa MLS, Major League Soccer, utakapoanza tena Machi 8.
Uhamisho huu unatarajiwa kuanza mara tu Dirisha la Uhamisho litakapofunguka Januari 1 na Bosi wa Fulham, Rene Meulensteen, ameupokea kwa furaha.
Dempsey alidumu na Fulham kwa Miaka Mitano na Nusu na kuichezea Mechi 184 na kufunga Bao 50
 
FULU VIWANJA