Social Icons

Pages

Monday, 16 December 2013

BEKI WA CROATIA, SIMUNIC, AFUNGIWA MECHI 10!!

FIFA Jana imemwadhibu Beki wa Croatia, Josip Simunic, kwa kumfungia Mechi 10, kumtwanga Faini Swiiss Franc 30,000 na kumpiga marufuku kuhudhuria Mechi yeyote ya Croatia wakati wa Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil Mwezi Juni.
FIFA imetoa Adhabu hiyo ya Kifungo cha Mechi 10, ambacho kinaanzia Mechi za Croatia za Fainali za Kombe la Dunia huko Brazil, baada ya Mchezaji huyo kupatikana na hatia ya kutoa Saluti ya Kibaguzi na Kifashisti mara baada Croatia kuibwaga Iceland kwenye Mechi ya Mchujo huko Ulaya ambayo iliwapa nafasi kwenda Brazil.
Simunic, mwenye Miaka 35 na ambae ni Nahodha wa Klabu ya Dinamo Zagreb, alifanya kosa hilo Novemba 19 wakati Croatia walipoifunga Iceland 2-0 na yeye kunaswa kwenye Video akitumia Kipaza Sauti kuimba Ubaguzi uliotumika wakati wa Utawala wa Kidhalimu na Kifashisti wa Masapota wa Nazi wa Ustase.
Katika Taarifa yake FIFA imesema Mchezaji huyo alitamka Saluti ya Kibaguzi iliyokuwa ikitumika wakati wa Vita Kuu ya Pili ikiwa ni kuvunja Kanuni ya Nidhamu ya FIFA ya 58 Aya ya 1a.
Adhabu hii kali ya FIFA inaonyesha nia thabiti ya kutokomeza Ubaguzi katika Soka.
 
FULU VIWANJA