Social Icons

Pages

Thursday, 12 May 2016

MKWANJA BORA DUNIANI: RONALDO JUU, LIONEL MESSI WA PILI, ROONEY WA 6, NDIE JUU ENGLAND!

KWA mujibu wa Jarida kabambe la Biashara la huko Marekani, Forbes, Cristiano Ronaldo ndie Mchezaji wa Soka anaepata Malipo ya juu kupita yeyote Duniani.
Ronaldo, ambae huichezea Real Madrid ya Spain, alivuna Dola Milioni 82 kwa Mwaka uliopita zikiwa Dola Milioni 53 kama Mshahara na Dola Milioni 29 Mapato yatokanoyo na Matangazo na Udhamini.
Forbes pia limethibitisha kuwa hivi sasa Ronaldo ndie Mwanamichezo anaelipwa vizuri kupita mwingine yeyote katika Michezo yote.
Anaemfuata Ronaldo ni Staa wa Barcelona Lionel Messi alievuna Dola Milioni 77 zikiwa Mshahara ni Dola Milioni 51 na Matangazo na Udhamini Dola Milioni 26.
Kwenye Listi hiyo ya Wachezaji wanaolipwa Mapato ya juu Kepteni wa Manchester United na England, Wayne Rooney, anakamata Nafasi ya 6 akiwa ndie wa kwanza wale Wachezaji wachezao Ligi England akivuna Jumla ya Dola Milioni 26.
FORBES – 20 BORA KWA WACHEZAJI WANAOLIPWA JUU:
1 Cristiano Ronaldo (Real Madrid): $82m
2 Lionel Messi (Barcelona): $77m (£53.3m)
3 Zlatan Ibrahimovic (Paris Saint-Germain): $37m
4 Neymar (Barcelona): $36m
5. Gareth Bale (Real Madrid) - $34m
6. Wayne Rooney (Manchester United) - $26m
7. Sergio Aguero (Manchester City) - $24m
8. Luis Suarez (Barcelona) - $23m
9. Eden Hazard (Chelsea) - $22m
10. Cesc Fabregas (Chelsea) - $21m
11. James Rodriguez (Real Madrid) - $21m
12. Yaya Toure (Manchester City) - $20m
13. Radamel Falcao (Chelsea) - $19m
14. Thiago Silva (Paris Saint-Germain) - $18m
15. Mesut Ozil (Arsenal) - $18m
16. Bastian Schweinsteiger (Manchester United) - $18m
17. Angel Di Maria (Paris Saint-Germain) - $18m
18. Robin van Persie (Fenerbahce) - $17m
19. David Silva (Manchester City) - $17m
20. Samir Nasri (Manchester City) - $15m
 
FULU VIWANJA