Social Icons

Pages

Thursday, 15 January 2015

COPPA ITALIANA: JUVE YAIFUMUA VERONA 6-1 IKO ROBO FAINALI KUCHEZA NA PARMA!


MABINGWA wa Italy, Juventus, wakicheza bila ya Nyota wao Carlos Tevez, Andrea Pirlo na Gigi Buffon, waliopumzishwa wakati Arturo Vidal akiwa mgonjwa, waliifumua Verona Bao 6-1 kwenye Mechi ya Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya Coppa Italiana.
Hadi Mapumziko Juve walikuwa mbele Bao 3-0 kwa Bao mbili za Sebastian Giovinco na moja la Roberto Pereyra.

Kipindi cha Pili, Paul Pogba akapiga Bao la 4 na kuifanya Juve iongoze 4-0 lakini Nene akafunga Bao kwa Verona na Gemu kuwa 4-1
Alvaro Morata akaipa Bao la 5 Juve kwenye Dakika ya 63 kwa Penati baada ya Rafael Marquez kumwangusha Sebastian Giovinco na la 6 kufungwa na Coman.

Juve sasa wametinga Robo Fainali na watacheza Nyumbani na Parma ambayo iliifunga Cagliari 2-1.
Mechi za Robo Fainali zitachezwa Februari 4.
 
FULU VIWANJA