Social Icons

Pages

Saturday, 12 April 2014

LIGI KUU ENGLAND: JUMAPILI MTANANGE LIVERPOOL v MAN CITY!! NAO CHELSEA KUIBWAGA SWANSEA HUKO LIBERTY STADIUM?



Jumapili 13 Aprili 2014
1537 Liverpool v Man City
1807 Swansea v Chelsea

LIVERPOOL v MAN CITY
Hii ni Bigi Mechi na pia muhimu katika mbio za Ubingwa kwani Liverpool wapo kileleni mwa Ligi Kuu England wakiwa Pointi 4 mbele ya Manchester City lakini wao wamecheza Mechi 2 zaidi.

LIGI KUU ENGLAND
MSIMAMO-Timu za Juu:
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
Liverpool
33
23
5
5
90
40
50
74
2
Chelsea
33
22
6
5
65
24
41
72
3
Manchester City
31
22
4
5
84
29
55
70
4
Arsenal
33
19
7
7
56
40
16
64
5
Everton
32
18
9
5
52
31
21
63
6
Tottenham Hotspur
33
18
5
10
45
45
0
59
7
Manchester United
33
17
6
10
56
38
18
57

Liverpool wanaingia kwenye Mechi hii wakiwa hawajafungwa katika Mechi 14 za Ligi, wameshinda 9 kati ya hizo, wakati Man City hawajafungwa katika Mechi 10 za Ligi za Ugenini.
Hali za Wachezaji
LIVERPOOL_V_MAN_CITYMeneja wa Liverpool Brendan Rodgers itabidi aamue kumchezaji yupi acheze Sentahafu kati ya Mamadou Sakho na Daniel Agger baada ya wote kupona maumivu yao lakini watamkosa Jose Enrique ambae bado kaumia ila Joe Allen anaweza kuanza ikiwa Rodgers ataamua anahitaji Kiungo wa ziada kwenye safu hiyo.
Man City wao wana faraja kubwa baada ya Mfungaji wao Bora Sergio Aguero, aliekosa Mechi 5, kupona na sasa yuko fiti kwa Mechi hii.
Lakini City itaendelea kumkosa Matija Nastasic ambae ana tatizo la Goti.
 
FULU VIWANJA