Social Icons

Pages

Saturday, 12 April 2014

Inter yamtaka Mikel, Morocco kucheza na Burkina Faso



MLINDA Mlango wa timu ya DR Congo, Robert Kidiaba anaamini jukumu lake jipya katika timu hiyo kama balozi wa amani, kunaweza kusaidia kuunganisha nchi yake sehemu mbalimbali duniani.
Golikipa huyo mwenye umri wa miaka 38, anaamini nchi yake haitakuwa na maendeleo bila kuwepo na amani.
Kwa miaka kadhaa, Congo imekuwa kwenye migogoro na kutokea mauaji ya kutisha kutokana na rasilimali kubwa za asili zilizopo nchini hapo.
 “Miaka mingi ya vita imetufanya tuchelewe kupata maendeleo ya nchi yetu, najua kwamba si rahisi kumshirikisha mtu katika mchakato wa amani hapa Congo, kwakuwa nchi imekuwa ikikabiliwa na vita,” alisema Kidiaba.
[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[[

SHIRIKISHO  la Soka nchini hapa FA, limesema timu yake ya Burkina Faso itacheza mechi ya kirafiki na timu ya Morocco, Mei 24 mwaka huu nchini Ureno.
Mwenyekiti wa shirikisho hilo, Sita Sangaré amesema kwenye mkutano w maandalizi ya kushiriki fainli za AFCON zitakazofanyika nchini Morroco mwakani.
Burkina Faso na Morocco zilishindwa kufuzu kushiriki fainali za kombe la Dunia mwaka huu, lakini upande huo ulisema kwamba timu yao haikuwa imara kushiriki fainali za Brazil.
Morocco bado haijapata kocha wakati ikijiandaa na Uchaguzi wa mwenyekiti wa Shirikisho hilo, Aprili 13 mwaka huu.



KLABU ya Inter Milan ya nchini ITALI,A imepanga kurejea nchini Englan kusaka wachezaji nyota, ambapo inamtizamia kiungo wa Chelsea, John Obi Mikel.
Rais wa Inter, Erick Thohir alikuwepo dimba la Stamford Bridge wakati The Blues ilipoizaba mabao 2-0 Paris Saint-Germain katika robo fainali ya Ligi ya Mabigwa iliyochezea juzi.
Kiungo huyo, amecheza mechi tisa za Ligi Kuu England chini ya kocha Jose Mourinho tangu aliporejea Chelsea, na ana uwezekano wa kutimkia Nerazzurri.
Thohir, amekuwa na mahusiano mazuri na klabu za Ligi England na amepanga kuwaleta wachezaji katika mji wa San Siro, majira ya joto.

 

Lassana Diarra


MWANASHERIA wa Kiungo wa Mali, Lassana Diarra na klaku za Real Madrid, Arsenal na Chelsea, Eric Dupond Moretti, amekanusha taarifa iliyodai kwamba mteja wake atajihusisha na Uasi nchini Syria.
Vyombo vya habari vya kijamii vilidai kwamba kiungo huyo wa zamani wa Ufaransa, ambaye anayeichezea klabu ya mjini hapa, Lokomotiv atakwenda mashariki ya Kati kumpinga rais Bashar Al-Assad.
“Diarra, hawezi kwenda Syria, na hawezi kuwa muasi bali ataendelea kuchezea mpira wa miguu,”alisema Eric Dupond Moretti.
 
FULU VIWANJA