Social Icons

Pages

Wednesday, 12 February 2014

aS CANNES YAMUWEKA KAPOMBE SOKONI RASMI, YATANGAZA DAU LAKE



Klabu ya AS Cannes inayoshiriki Ligi Daraja la Nne nchini Ufaransa, hatimaye imenyoosha mikono na kutangaza kumuuza beki wake Shomari Kapombe.

Uongozi wa AS Cannes umesema bei ya Kapombe ambaye bado yuko hapa nchini ni euro 70,000 (Sh milioni 154) huku ikitaja majina ya klabu mbili, Yanga na Azam FC wanakaribishwa kuanza mazungumzo.

Awali, tuli pata taarifa za ndani kuhusiana na uamuzi huo, lakini uongozi ukawa mgumu kulizungumzia.

Lakini jana mchana, mmoja wa viongozi wa AS Cannes, Pierre Pilorget alizungumza na alisema wamefikia uamuzi huo na klabu za Tanzania zilizokuwa zinamtaka zinaweza kufanya mazungumzo na wakala wake au klabu hiyo.
“Waambie Yanga kuwa sasa Kapombe tumemuweka sokoni, wanaweza kumpata na bei ndiyo hiyo. Kama tulivyosema awali wasipite njia za mkato.
“Njia nzuri ni kufika kwetu na kuzungumza, wakiona hawawezi kufanya hivyo wazungumze na wakala wake naye atafika kwetu,” alisema Pilorget.
Alipoulizwa jana kutoka Uholanzi, wakala wake Denis Kadito alisema angependa kuliacha suala hilo lizungumziwe na klabu.
“Tukianza kuzungumza wote tutachanganya mambo, nafikiri tuiache klabu ndiyo ilizungumzie suala hilo,” alisema Kadito.
Simba ilimpeleka Kapombe AS Cannes bila ya malipo huku ikusubiri kama atauzwa, itapata asilimia 40 ya mauzo yake.
 
FULU VIWANJA