Social Icons

Pages

Tuesday, 14 January 2014

MOYES ATUA JUVE YEYE MWENYEWE KUOMBA KUSAJILI WAWILI, POGBA NA VIDAL

KOCHA David Moyes alifanya mazungumzo na muhusika mkuu wa mijadala ya usajili wa Juventus baada ya kupanga kuwachukua Paul Pogba na Arturo Vidal.
KOcha huyo wa Manchester United alikutana bosi wa bodi, Beppe Marotta baada ya mchezo wa Juventus na Cagliari Jumapili na kujadiliana juu ya uwezekano wa aidha kuwasaini wote kati ya wachezaji hao anaowataka sana.
Baada ya kusafiri hadi Cagliari na kocha wa kikosi cha kwanza, Jimmy Lumsden kushuhudia Juve wakitoka nyuma kwa bao 1-0 na kushinda 4-1 na kuendelea kuongoza msimamo wa ligi ya Italia, Serie A, Moyes aliweka wazi mipango yake ya kusajili kutoka klabu ya Turin. 
Lakini hadi anarejea Manchester, alilazimika kukubali kwamba anaweza kumrejesha Pogba pekee Old Trafford na kuhusu Vidal asubiri hadi mwisho wa msimu.
Macho pima: Kocha wa Manchester United, David Moyes alisafiri hadi Italia kuwaangalia vigogo wa Italia Jumapili
Juventus midfielder Paul Pogba
Juventus midfielder Arturo Vidal
Walengwa: Manchester United ipo kwenye mazungumzo na Juve ili kuwasajili viungo Paul Pogba (kushoto) na Arturo Vidal 

Zinedine Zidane aliwahi kusema kuondoka kwa Pogba United miezi 18 iliyopita lilikuwa ni kosa kubwa alilolifanya kocha wa zamani wa klabu hiyo, Sir Alex Ferguson’s, lakini Moyes anapambana kumrejesha mkali huyo.
Paris St-Germain pia inamtaka Pogba na wanaonekana wako tayari kutoa dau linalotakiwa la Pauni Milioni 40 kumnasa. Inafahamika alikuwa tayari kwenda PSG, lakini hajakataa kurejea Old Trafford.
Kwa sasa, Juventus wako wazi wanasema hawamuuzi mchezaji huyo. "Kwa upande wetu, hatutakia kumuuza Pogba na zaidi tumefunga milango juu ya uwezekano wowote wa mtu kutaka kununua mchezaji kwetu,"
 
FULU VIWANJA