Social Icons

Pages

Wednesday, 15 January 2014

KOCHA MPYA KUANZA KUIONA YANGA IKICHEZA MECHI YA KIRAFIKI LEO


Kocha Mkuu mpya wa Yanga, Hans van Der Pluijm, raia wa Uholanzi, amesema anataka soka la kasi huku kikosi chake kikicheza kwa ushirikiano katika kushambulia na kukaba.

Van Der Pluijim (64), amemueleza mmoja wa viongozi wa Yanga kwamba ana imani siku chache atakazokaa na timu nchini Uturuki, atafanya mabadiliko huku akiahidi kuwatumia Mrisho Ngassa, Emmanuel Okwi na Simon Msuva katika aina ya ushambuliaji wa kasi anaoutaka.
 “Kocha kasema anapenda soka la kasi, tumemueleza kuhusu wachezaji kadhaa wenye aina hiyo, amefurahia. Unajua alitaka kujua baadhi ya mambo, mfano alitaka kujua kama tuna wachezaji wenye kasi, tumemtajia Ngassa, Okwi, Msuva na amesema pia anataka timu inayocheza kwa ushirikiano. Lakini naamini ataanza na safu ya ulinzi,” alisema kiongozi huyo.
“Ana mambo mengi anataka kufanya, lakini ametaka kwanza kuiona timu, vizuri atawaona wakicheza mechi kwa kuwa atafika kesho (leo), halafu saa chache watacheza mechi. Atapata nafasi ya kuwaona.”
Kocha huyo Mholanzi, amekuwa akisifiwa kwa soka la nguvu wakati akiifundisha Berekum Chelsea ya Ghana na alipofanya mahojiano mafupi na waandishi  alisisitiza suala la subira.
 
FULU VIWANJA