Social Icons

Pages

Tuesday, 31 December 2013

LEWANDOWSKI KUTANGAZA JANUARI 2 KLABU IPI ATAHAMIA!


LEWANDOWSKI-SHUJAAROBERT LEWANDOWSKI, Straika hatari kutoka Poland anaechezea Borussia Dortmund huko Germany, atatangaza rasmi Klabu ipi atahamia hapo Januari 2.
Hilo ni kwa mujibu wa Mtangazaji wa Kituo kimoja cha TV huko Poland, Mateusz Borek, ambae alitoboa habari hizi kwenye Mtandao wa Twitter mara tu baada ya Lewandowski kurushwa kwenye Kipindi cha Mtangazaji huyo, 'Football Café', na kufanya habari hizo ziwe za kuaminika.
Mkataba wa sasa wa Lewandowski na Borussia Dortmund unamalizika mwishoni mwa Msimu na hilo linamfanya Staa huyo awe huru kuanzia Januari 1, kwa mujibu wa FIFA, kufikia makubaliano ya awali, kabla kusaini Mkataba wa Kudumu, na Klabu yeyote nyingine inayomtaka kumnunua.
Inaaminika Mchezaji huyo atahamia kwa Mabingwa wa Bundesliga, Ulaya na Dunia, Bayern Munich, ingawa mwenyewe hajathibitisha hilo hadi sasa na hivyo kuacha mlango wazi kwa kila uvumi kuzagaa.
Klabu kadhaa Vigogo Barani Ulaya zimekuwa zikimwinda Straika huyo hatari kwa Magoli na Siku za nyuma amekuwa akihusishwa sana na kuhamia Manchester United, Barcelona na Real Madrid.
 
FULU VIWANJA