Social Icons

Pages

Thursday, 19 December 2013

JACK WILSHERE AKIRI KOSA, APINGA KIFUNGO MECHI 2


WILSHERE_KIDOLW_JUU-17DECKIUNGO wa Arsenal Jack Wilshere amekiri Shitaka la Utovu wa Nidhamu toka kwa FA, Chama cha Soka England, baada kunaswa akitoa ishara ya Kidole kimoja ambayo huchukuliwa kama matusi wakati Arsenal inapigwa Bao 6-3 na Manchester City Jumamosi Uwanjani Etihad lakini amepinga Adhabu ya Kufungiwa Mechi 2 ambayo moja kwa moja huambatana na kosa la aina hiyo.
Tukio hilo ambalo lilitokea katika Dakika ya 67 halikuonwa na Refa Martin Atkinson lakini FA, chini ya taratibu zake mpya za Msimu huu, Jopo la Marefa Watatu wa zamani wamelipitia na kuamua lingestahili Kadi Nyekundu kama Refa angeliliona.
Kesi ya Wilshere itasikizwa na Kamisheni ya Nidhamu ya FA hii leo.

MECHI ZIJAZO ZA ARSENAL:
23 Decemba Chelsea (Emirates)
26 Decemba West Ham (Upton Park)
29 Decemba Newcastle (St James Park)
1 Januari Cardiff City (Emirates)

Ikiwa Kamisheni hiyo itamwona na hatia basi atazikosa Mechi za Arsenal hapo Desemba 23 dhidi ya Chelsea Uwanjani Emirates na ile ya Desemba 26 huko Upton Park na West Ham.
Hapo Desemba 2011, Luis Suarez alifungiwa Mechi moja na kupigwa Faini £20,000 baada ya kuwaonyeshea ishara kama hii ya Wilshere Mashabiki wa Fulham.www.fulu viwanja blogspot.com
 
FULU VIWANJA