Social Icons

Pages

Tuesday, 17 December 2013

BAYERN MUNICH YATINGA FAINALI KATIKA FAINALI YA MASHINDANO YA FIFA YA VILABU

MABINGWA wa Ulaya, Bayern Munich, Usiku wa jana huko Stade Adrar, Agadir, Nchini Morocco wameitandika Guangzhou Evergrande FC Bao 3-0 kwenye Mechi ya Nusu Fainali ya Mashindano ya FIFA ya Kombe la Dunia kwa Klabu.
Hadi Haftaimu, Bayern Munich walikuwa mbele kwa Bao 2-0 kwa Bao za Franck Ribery, Dakika ya 40 na Marijo Mandzukic, Dakika ya 44.
Kipindi cha Pili, kwenye Dakika ya 47, Mario Goetze aliipa Bayern Bao la 3 na kutinga Fainali ambayo watakutana na Mshindi wa Nusu Fainali nyingine kati ya Wenyeji Raja Casablanca na Atlético Mineiro ya Brazil.
Kabla ya Mechi hiyo itachezwa Mechi ya kusaka Mshindi wa 5 kati ya Al Ahly na Monterrey.

 
FULU VIWANJA