Social Icons

Pages

Monday, 23 December 2013

ADEBAYOR AIPONDA SPURS


Jumapili, Emmanuel Adebayor alifunga Bao mbili katika Mechi yake ya kwanza kuanza kucheza kwenye Ligi Kuu England Msimu huu wakati Spurs inaichapa Southampton Bao 3-2.
Lakini Adebayor, mwenye Miaka 29, amekasirishwa na kitendo cha Klabu hiyo kutomhusisha kwenye Picha rasmi ya Wachezaji wa Klabu hiyo na pia kutengwa kufanya Mazoezi na Kikosi cha Kwanza wakati Meneja akiwa ni Andre Villas-Boas kabla hajatimuliwa Wiki moja iliyopita.ADEBAYOR-SPURS
Adebayor ameeleza: “Ilikuwa ngumu. Nikija Mazoezini naiona Picha ya Timu na mie simo, huko ni kunivunjia heshima.”
Katika Msimu wa 2011/12, Adebayor alichezea Tottenham kwa Mkopo akitokea Man City na kufunga Bao 17 katika Mechi 33 na Agosti 2012 alijiunga moja kwa moja na kuwa Mchezaji wa kudumu wa Tottenham kwa Dau la Pauni Milioni 5.
Katika Msimu uliofuatia wa 2012/13, Adebayor aliifungia Tottenham Bao 9 tu katika Mechi 36 na Msimu huu alicheza Dakika 45 tu chini ya Villas-Boas.
Adebayor amesema: “Mie ni Mchezaji wa Kulipwa, ilibidi nijikaze na kufanya nilichoamriwa. Walitaka nifanye Mazoezi na Rizevu, nilifanya kwa furaha na walinitaka nifanye Mazoezi peke yangu, nilifanya kwa furaha.”
Ameongeza: “Sasa kila kitu kinaenda sawa. Nilifanya bidii na sasa naona matunda. Nimefurahi.”
Baada kutimuliwa Villas-Boas, Tim Sherwood ameshika wadhifa kwa muda kuanzia Wiki iliyopita na mara moja akamrudisha Adebayor Kundini na katika Mechi ya kwanza tu chini ya Sherwood, Jumatano iliyopita kwenye Capital One Cup, Adebayor aliifungia Spurs Bao 1 lakini wakafungwa na West Ham 2-1 na kutolewa nje ya Kombe hilo.
Katika Mechi iliyofuatia, hapo Jana, Adebayor alichezeshwa Mechi yake ya Ligi ya kwanza dhidi ya Southampton na kupiga Bao 2 na Spurs kuifunga Southampton Bao 3-2.www.fulu viwanja blogspot.com
 
FULU VIWANJA