Social Icons

Pages

Wednesday, 27 November 2013

VIDIC, VAN PERSI NJE KATIKA MECHI YA LEO

VIDIC, VAN PERSIE KUIKOSA LEVERKUSEN!


>>MSIMU HUU BAYARENA: LEVERKUSEN WAMESHINDA ZOTE KASORO SARE NA BAYERN!!
NAHODHA Nemanja Vidic na Robin van Persie wataikosa Mechi ya Manchester United huko BayArena dhidi ya Bayer Leverkusen ya Kundi A la UCL, UEFA CHAMIONZ LIGI.
Meneja David Moyes amethibitisha kukosekana kwao na wote hawakuwemo kwenye Kikosi kilichosafiri leo kutoka Jiji la Manchester kwenda huko Germany.
Licha ya Vidic kufanya Mazoezi Asubuhi hii, Moyes amesema: “Wote bado wana maumivu. Wote si maumivu ya muda mrefu lakini hawapo tayari kwa sasa.”

MSIMAMO:
KUNDI A
NA
TIMU
P
W
D
L
F
A
GD
PTS
1
Manchester United
4
2
2
0
6
3
3
8
2
Bayer 04 Leverkusen
4
2
1
1
8
5
3
7
3
FC Shakhtar Donetsk
4
1
2
1
3
5
-2
5
4
Real Sociedad
4
0
1
3
1
5
-4
1

NEMANJA_VIDIC-KAPITANEHata hivyo, Man United itafarijika kwa kurudi tena Kikosini kwa ‘kiraka’ Phil Jones ambae alikuwa nje kwa maumivu ya nyonga lakini itawakosa Michael Carrick, ambae ni Majeruhi, na Marouane Fellaini, ambae yupo Kifungoni kwa Mechi moja baada ya Kadi Nyekundu katika Mechi iliyopita ya Kundi A la UCL walipotoka Sare na Real Sociedad huko Spain.
Hii ni Mechi ngumu kwenye Kundi A ambayo Mshindi wake ndie atakaefuzu kusonga Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ingawa kwa Man United hata Sare kwao si mbaya.
Wakiwa kwao BayArena Msimu huu, Bayer Leverkusen wameshinda Mechi zao zote kasoro moja dhidi ya Mabingwa wa Germany na Ulaya, Bayern Munich, ambayo walitoka Sare.

 
FULU VIWANJA