Social Icons

Pages

Friday, 15 November 2013

URENO WASHINDA,UFARANSA HOI

PORTUGAL 1 SWEDEN 0
Cristiano Ronaldo Jana alifunga Bao katika Dakika ya 82 na kuwapa Portugal ushindi wa Bao 1-0 walipocheza na Sweden katika Mechi ya kwanza ya Mchujo ya kusaka Timu 4 za mwisho za Ulaya kwenda huko Brazil Mwakani kwenye Fainali za Kombe la Dunia.
Bao hilo lilifungwa katika Dakika ya 82 kwa kichwa cha chini ya Ronaldo alipounganisha krosi ya Miguel Veloso.
Sweden, waliokuwa wakicheza kitimu walipatia nafasi kadhaa kupitia Johan Elmander, Sebastian Larsson na Kim Kallstrom huku Nyota wao mkubwa Zlatan Ibrahimovic akishindwa kupiga hata shuti Golini akiwa ndani ya Boksi.
UKRAINE 2 FRANCE 0
Bao za Roman Zozulya, Dakika ya 61, na Andriy Yarmolenko, Penati Dakika ya 83, zimewapa ushindi Ukraine wa Bao 2-0 walipocheza na France huko Kiev hapo Jana.
Hili ni pigo kubwa kwa France ambao sasa wako hatarini kuzikosa Fainali za Kombe la Dunia kwa mara ya kwanza katika Miaka 20
Katika Dakika za Majeruhi Beki wa France Laurent Koscielny na Oleksandr Kucher walitolewa kwa Kadi Nyekundu.
 
FULU VIWANJA