Social Icons

Pages

Thursday, 14 November 2013

CHILE USO KWA USO NA THREE LION(ENGLAND)

NAHODHA wa England Steven Gerrard pamoja na Beki Kyle Walker wataikosa Mechi ya Nchi yao na Chile hapo Ijumaa baada ya kupata maumivu kidogo lakini wanatarajiwa kucheza Mechi ya Jumanne dhidi ya Germany.
Wakati Gerrard bado anajiuguza tatizo la Paja aliloumia wakati Klabu yake Liverpool inaifunga Fulham Wikiendi iliyopita, Kyle Walker alikosa Mazoezi ya England hapo Jumatano akiwa na tatizo la Mguu na hii inafuatia kujitoa kwenye Kikosi Wachezaji wawili wa Manchester United, Michael Carrick na Danny Welbeck, ambao wameumia.
Mbali ya Majeruhi hao, Kambi ya England pia ilivurugika mwanzoni tu baada ya kulazimika kubadilisha Kituo chao cha kawaida toka National Football Centre kwenda Watford kukimbia kuambukizwa Ugonjwa wa Tumbo uliozuka kwenye Kituo hicho chao cha kawaida.
Wakati huo huo, Fowadi wa Chile anaechezea Klabu ya Barcelona, Alexis Sanchez, amewasha moto wa Mechi kati ya England na Chile pale alipotamka Wachezaji wa England wako ‘laini’ kutokana na Maisha yao ya kudekezwa na hilo limepokewa vibaya toka Kambi ya England.
Straika wa Southampton, Rickie Lambert, amesema sasa hawahitaji tena motisha toka kwa Meneja wao kwani kauli hiyo ya Sanchez imewakera.
Lambert ametamka: “Kwa kauli ile huhitaji motisha tena!”
 
FULU VIWANJA