Social Icons

Pages

Monday, 25 November 2013

GUS POYET ATAKA KADI YA WES BROWN IFUTWE

GUS POYET ATAKA KADI NYEKUNDU YA WES BROWN IFUTWE!


>> POYET: “NATAKA CHAMA CHA MAREFA KITUOMBE RADHI!”
GUS_POYETMENEJA wa Sunderland Gus Poyet ametaka Kadi Nyekundu aliyopewa Beki wake Wes Brown kwenye Mechi waliyofungwa Jana 2-0 na Stoke City ifutwe na Mkuu wa Marefa Mike Riley awaombe radhi.
Refa wa Mechi hiyo ya Ligi Kuu England, Kevin Friend, alimtoa nje Wes Brown kwa madai alimchezea faulo Charlie Adam lakini ukweli ni kuwa Mchezaji huyo wa Stoke City hakuguswa na Brown aliucheza Mpira tu.
Wiki iliyopita, Mike Riley, Mkuu wa Marefa, alimpigia Simu Meneja wa West Bromwich Albion, Steve Clarke, na kumwomba radhi baada ya Refa Andre Marriner kuwapa Chelsea Penati tata katika Dakika ya 94 na kusawazisha Bao na Mechi kwisha 2-2.
Poyet amesema: “Labda itabidi Mike Riley anipigie Simu. Nitaacha Simu yangu wazi.”
Tukio la kutolewa kwa Wes Brown lilitokea baada ya Sunderland kufungwa Bao 1-0 Mfungaji akiwa Charlie Adam na wakati huo Poyet alichukizwa sana na kuwapigia kelele Marefa.
Poyet ameeleza: “Ama tuombwe Msamaha na Kadi ifutwe. Tutakubali kosa la Refa na kusonga mbele!”
Aliongeza: “Ni ngumu kuelewa. Labda Mtu anieleze kwa maneno mengine. Sidhani kama yapo maelezo! Je ilikuwa rafu ya Miguu miwili? Hapana. Alikuwa hamiliki Mpira? Hapana. Je alipitisha Mguu juu ya Mpira? Hapana. Je mpinzani alikuwa hatarini? Hapana. Alimgusa? Hapana. Tafadhali nieleze. Ni ngumu kukubali!”
Poyet alimalizia: “Nataka Chama cha Marefa kituombe radhi! Walimpigia Simu Meneja wa Kiingereza na nadhani sasa ni wakati wa kumpigia Meneja wa Nje!!”
 
FULU VIWANJA