Social Icons

Pages

Thursday, 14 November 2013

CECAFA KUPANGA MAKUNDI KESHO

CECAFA_LOGO12DROO ya kupanga Makundi ya Mashindano ya Chalenji Cup yatakayochezwa Nchini Kenya sasa zitafanyika lIjumaa Mjini Nairobi kama ilivyothibitishwa leo hii na Afisa Habari wa CECAFA, Rogers Mulindwa.
Afisa huyo amefafanua kuwa zipo Nchi kadhaa ambazo bado zinasubiriwa kuthibitisha ushiriki wao na pia udhamini wa Mashindano hayo yatakayochezwa kuanzia Novemba 27 hadi Desema 12 utaanuliwa rasmi Siku hiyo hiyo ya Ijumaa.
Vile vile, CECAFA imesema kuwa ile mipango ya awali ya baadhi ya Mechi kuchezwa huko Kisumu na Mombasa sasa umefutwa na Mechi zote zitachezwa Nairobi ingawa bado upo uwezekano wa baadhi ya Mechi kuchezwa Miji mingine.
Wakati huo huo, Mabingwa Watetezi wa Chalenji Cup, Uganda, ambayo ipo chini ya Kocha Milutin ‘Micho’ Sredojevic, imethibitisha kuwa Kikosi chake cha kutetea Taji lake kitaundwa na Wachezaji wanaocheza Soka lao ndani ya Uganda tu ikiwa ni Mazoezi yao ya ushiriki wao kwenye Fainali za CHAN zitakazochezwa Mwezi Januari huko Afrika Kusini, Mashindano ambayo Kanuni yake ni kuchezesha Wachezaji wale tu wanaocheza ndani ya Nchi zao.
Michuano ya Mwaka huu ya Chalenji Cup inatarajiwa kushirikisha Nchi zote 12 ambazo ni Wanachama wa CECAFA pamoja na Waalikwa Zambia na Malawi.

Wanachama wa CECAFA, Shirikisho la Soka kwa Nchi za Afrika Mashariki na Kati, ni Wenyeji wa Mashindano haya Kenya, Uganda, Tanzania Bara, Zanzibar, Rwanda, Sudan, Burundi, South Sudan, Ethiopia, Eritrea, Djibouti na Somalia.
Mechi za Chalenji Cup Mwaka huu zitarushwa moja kwa moja na Vituo vya TV vya SuperSport, TV ya Taifa ya Uganda na TBC.
 
FULU VIWANJA