Mvuto kwa El Clasico hii ni Klabu zote
mbili kuwa na Wachezaji wapya ambao wanaweza kucheza kwa mara ya kwanza
kwenye mtanange wa aina hii kwa Barcelona kumchezesha Mchezaji mpya
Neymar waliemnunua Msimu huu kutoka Santos ya Brazil na Real kumtumia
Gareth Bale alievunja Dau la kununuliwa kwa Bei Ghali Duniani
walipomnunua kwa Euro Milioni 100 kutoka Tottenham.
Lakini wakati Neymar akionyesha cheche
zake kwenye Timu ya Barcelona, Bale amekuwa akikumbwa na Majeruhi
yaliyomfanya acheze Mechi chache tu.
Kocha wa Real, Carlo Ancelotti,
amedokeza kuwa Bale ataanza Mechi hii pamoja na Wachezaji wake wapya
wengine Isco na Asier Illarramendi huku Cristiano Ronaldo akiongoa
majeshi.
Nae, Gerardo Martino, amedokeza kuwa
mashambulizi ya Kikosi chake yataongozwa na Lionel Messi na Neymar huku
ukiwepo uwezekano wa Beki wao Mkongwe ambae pia ni Nahodha wao, Carles
Puyol, kuanza Mechi hii baada ya kurudi tena dimbani akiwa nje
akijiuguza Goti lake tangu Mwezi Machi.
MECHI ZA MWISHO:
02-03-2013 Real Madrid: 2 FC Barcelona: 1 [La Liga]
26-02-2013 FC Barcelona: 1 Real Madrid: 3 [Copa Del Rey]
30-01-2013 Real Madrid: 1 FC Barcelona: 1 [Copa Del Rey]
07-10-2012 FC Barcelona: 2 Real Madrid: 2 [La Liga]
29-08-2012 Real Madrid 2 FC Barcelona 1 [Super Cup]
23-08-2012 FC Barcelona 3 Real Madrid 2 [Super Cup]