Social Icons

Pages

Wednesday, 30 March 2016

PLUIJM ATAKA YANGA IPEWE HESHIMA YA UTAIFA, ASEMA HAIWAKILISHI YANGA TU PLUIJM

MABINGWA watetezi wa Tanzania Bara, Yanga SC, wana jukumu la kuivaa Al Ahly ya Misri katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.

Mechi ya kwanza inatarajiwa kupigwa Aprili 9 jijini Dar es Salaam, halafu zitarudiana jijini Cairo katika mechi ambayo kama hakutakuwa na dira ya nani aliyefanya vizuri, majibu yatapatikana katika mechi hiyo.

Yanga imefikia hatua ya pili baada ya kuvuka ile ya awali na ya kwanza kwa kuzitoa Cercle de Joachim ya Mauritius na baadaye APR ya Rwanda. Sasa inakutana na wababe wa Afrika ambao wamekuwa katika kipindi cha mpito. Sasa angalau wanaonekana kuanza kukaa sawa.

Hakuna ubishi haitakuwa kazi rahisi kwa Yanga na kocha wake mkuu, Hans van der Pluijm, anakiri kwamba wana kazi kubwa na wanatakiwa kufanya kazi kwa ubora wa juu zaidi ya mechi nne za Ligi ya Mabingwa Afrika walizocheza.
 
FULU VIWANJA