
Sir Alex Ferguson alistaafu kuwa Meneja wa Manchester United Mwezi Mei Mwaka Jana baada ya kuendesha himaya yake kwa mafanikio makubwa kwa Miaka 26.
Toleo hili jipya litaongeza habari za maisha ya Sir Alex tangu astaafu pamoja na mawazo yake kuhusu Manchester United alivyoiona baada ya kustaafu na hasa himaya fupi ya Miezi 10 ya Meneja aliemrithi yeye, David Moyes, ambayo iliivuruga Man United na kuipotezea Ubingwa na pia kuifanya ishindwe kucheza Ulaya kwa mara ya kwanza tangu 1996 baada ya kumaliza Nafasi ya 7 kwenye Ligi Kuu England.
Pia Toleo hilo jipya litagusia mafundisho yake huko Chuo Kikuu cha Harvard Marekani, Usiku wa Tuzo za Oscar na Tripu yake ya Boti kuzunguka Hebrides, Magharibi ya Pwani ya Scotland.
Hadi sasa hamna fununu yeyote nini kitaandikwa kwenye Toleo hilo jipya, hasa kuhusu kushindwa kwa David Moyes, ambae yeye mwenyewe Sir Alex ndie aliempendekeza.
Hivi sasa Man United ipo chini ya Meneja mpya Louis van Gaal ambae ametoboa yeye na Sir Alex ni Marafiki na wakati wowote ule watakutana kupata Kahawa au Mvinyo pamoja.
Hata hivyo, haijajulikana kama pia Van Gaal nae atatajwa kwenye Toleo hili jipya la Kitabu cha Sir Alex Ferguson, 'My Autobiography