

Wachezaji walioteuliwa ni wale wanaocheza Ulaya na Scolari amesema ataongeza Wachezaji watatu wanaocheza Klabu za Nchini Brazil.
Brazil inatarajiwa kutangaza Kikosi chao
kitakachocheza Fainali za Kombe la Dunia zitakazochezwa Nchini kwao
hapo Mei 7 na wao watacheza Mechi ya Ufunguzi ya Fainali hizo hapo Juni
12 dhidi ya Croatia.
Baada ya Mechi na South Africa, Brazil itacheza Mechi mbili za Kirafiki kati ya Juni 3 na 6.
Kuhusu Kipa Cesar, ambae hajacheza Mechi
akiwa na Klabu yake QPR ya England, Scolari amesema anategemea Kipa
huyo kupata Mechi nyingi na Klabu yake mpya inayocheza MLS huko
Marekani, Toronto, ambayo Wiki iliyopita amehamia kwa Mkopo.
Wachezaji wapya ambao wamo kwenye Kikosi
cha Brazil ni Beki wa Bayern Munich, Rafinha, na Kiungo wa Manchester
City, Fernandinho.
Chelsea imetoa Wachezaji watatu ambao ni Oscar, Ramires na Willian.
KIKOSI CHA BRAZIL:
KIPA: Julio Cesar (QPR/ENG)
MABEKI: Thiago Silva
(Paris SG/FRA), David Luiz (Chelsea/ENG), Dante (Bayern Munich/GER),
Dani Alves (FC Barcelona/ESP), Rafinha (Bayern Munich/GER), Marcelo
(Real Madrid/ESP)
VIUNGO: Paulinho
(Tottenham/ENG), Fernandinho (Manchester City/ENG), Luiz Gustavo
(Wolfsburg/GER), Ramires (Chelsea/ENG), Oscar (Chelsea/ENG), Willian
(Chelsea/ENG)
MASTRAIKA: Neymar (Barcelona/ESP), Hulk (Zenit St Petersburg/RUS), Bernard (Shakhtar Donetsk/UKR).